Search This Blog
Saturday, October 23, 2021
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha maradhi mbalimbali bali pia mwonekano wako unakuwa si mzuri. Makala haya yanaeleza namna ya kupunguza unene ndani ya siku saba.
Siku ya 1: Asubuhi kula matunda (lakini usile ndizi). Mchana chemsha kabichi, weka chumvi kidogo na nyanya, chemsha na upate supu. Kula mchanganyiko huo na utajiona umeshiba. Jioni kula tikiti maji na mbogamboga au kabichi uliyotengeneza mchana.
Siku ya 2: Kula mboga za majani asubuhi (usile mboga za majani zenye wanga kama karoti). Mchana kula kabichi iliyochemshwa, tengeneza na kachumbari. Katika kabichi weka chumvi, pilipili na mafuta ya olive. Jioni unaweza kula mlo kama wa mchana lakini unaweza kukaanga mboga nyingine za majani.
Siku ya 3: Kula mboga za majani na matunda, unaweza kuongeza kiazi kitamu kimoja.
Siku ya nne 4: Kula ndizi moja na unywe na maziwa ya mtindi wakati wa asubuhi. Mchana kula kabichi kama ulivyoitengeneza kwenye siku ya kwanza, usiku rudia mlo wa mchana.
Siku ya 5: Kula nyanya nne pamoja na samaki au kipande cha kuku asubuhi. Mchana unaweza kula samaki wa kuchemsha kiasi ambaye amechanganywa na nyanya. Wakati wa jioni unaweza kula chakula kama cha mchana.
Siku ya 6: Unaweza kula chakula cha protini na mboga za majani. Anza kwa kula kachumbari asubuhi. Mchana kula tambi kiasi na kipande kidogo cha samaki. Usiku tengeneza supu ya kabichi.
Siku ya 7: Anza kwa matunda na juisi. Mchana kula mboga za majani na usiku kula supu ya kabichi na kiazi kimoja.
Kumbuka: Unatakiwa kunywa maji angalau glasi nne kila siku. Usiendelee kwa muda mrefu, kumbuka dayati hii ni ni kwa siku saba. pekee.
Kitendawili cha Lissu, Lema kurejea Tanzania
Wakati Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Godbless Lema akidokeza mpango wake wa kurejea nchini kuendelea na siasa, makamu mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu amesema sababu zilizomfanya aondoke hazijaondoka bado zipo.
Kurejea kwa viongozi hao ambako kumeibuka mtandaoni huenda ukakiongezea nguvu chama hicho ambacho kwa sasa Mwenyekiti wake Freeman Mbowe yuko rumande akiendelea na kesi yake inayomhusisha makosa ya ugaidi.
Kutokuwepo viongozi hao mara kadhaa umetajwa kupunguza hamasa ya siasa kwa chama kikuu cha upinzani nchini na kusitisha programu zake kadhaa.
Hakikisho la Lema
Akizungumza juzi katika mitandao ya jamii, Lema aliyeondoka nchini baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 alisema anatafakari kufanya uamuzi wa kurejea Tanzania kuungana na ndugu zake, akisema majadiliano kuhusu hatua hiyo anayaanza hivi sasa.
“Nafanya uamuzi wa kuwepo Tanzania lini? Naanza sasa majadiliano na Mungu, familia na chama changu ili kufanya kazi pamoja. Nahitaji kuwa uwanjani (Tanzania) kuliko wakati wowote ule, nitakuwa tayari kukabiliana na matokeo yoyote,” alisema Lema.
Lema ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, alieleza hayo katika mtandao wa Club House unaowakutanisha wadau mbalimbali kwa ajili ya kujadili na kutoa maoni kuhusu mada inayowekwa mezani katika siku husika.
Kwa sasa Lema ambaye aliyekuwa mbunge wa Arusha Mjini anaishia nchini Canada alikopata hadhi ya ukimbizi wa kisiasa akitokea Nairobi, Kenya.
Katika mtandao huo, Lema alisema, “nafikiria nahitaji kumuona mwenyekiti (Freeman Mbowe) jela, akiwa mahabusu au mahakamani. Nahitaji kumtia matumaini, nahitaji vitu vingi kuhusu nyumbani, nipo tayari kwa lolote kabisa,” alisema Lema.
Lema aliwataka viongozi wa Chadema kusimama imara katika usimamizi wa kesi ya Mbowe, akisema mazingira ya kesi hiyo ni magumu.
Wakati, Lema akisema hayo, kiongozi mwenzake anayeishi nchini Ubelgiji Tundu Lissu alisema sababu zilizomkimbiza Tanzania kwenda ughaibuni bado hazijabadilika.
Lissu aliondoka nchini kwa mara ya kwanza Septemba 7, 2017 na kuelekea Nairobi, Kenya akiwa mahututi, baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana jijini Dodoma.
Mwaka 2018 alihamishiwa nchini Ubeligiji kwa matibabu zaidi hadi mwaka 2020 aliporejea nchini na kugombea urais, kabla ya kurejea tena Ubelgiji akidai kutishiwa maisha yake.
Akizungumzia hoja zilizoibuka mtandaoni baada ya mchungaji mmoja kuonekana akimkaribisha nyumbani, Lissu alisema “mtandaoni kuna Tundu Lissu wengi, huyo anayeelezwa na pastor (jina tunalihifadhi kwa sababu hatukumpata), sio yule Tundu Lissu aliyeko uhamishoni.
Alipotakiwa kufafanua kauli yake, Lissu alisema: “Sababu zilizonikimbiza Tanzania hazijabadilika. Wauaji bado wako huru mitaani na hakuna mpango wa kuwatafuta na kuwashughulikia kwa mujibu wa sheria.’’
Songwe kuwasaka watoto 1,000 waliokimbia shule
Mkuu wa wilaya ya Songwe, Simon Simalenga amesema wamejipanga kuanzisha oparesheni ya kuwasaka watoto zaidi ya 1,000 ambao hawafiki shuleni ili kukomesha tatizo la utoro kwenye shule za msingi zilizopo katika halmashauri ya Songwe mkoani Songwe.
Simalenga ametoa kauli hiyo Oktoba 21 kwenye kikao cha baraza la madiwani cha robo ya kwanza katika mwaka wa fedha 2021/22
Amesema atahakikisha wazazi wa watoto hao wanasakwa ili waweze kuwahamasisha watoto wao kuendelea na masomo.
“Siwezi kukubali watoto zaidi ya 1,000 kutofika shule lazima wazazi wa watoto hawa wafuatiliwe ambapo amesema atahakikisha watoto wote wanaozurura wanakamatwa na kurudishwa shuleni,” alisema Simalenga.
Simalenga amewaomba madiwani wa halmshauri hiyo kuhakikisha wanakaa na wazazi na kuwaeleza umuhimu wa elimu ili kukomesha suala la utoro na kujenga taifa lililo salama kwamadai mtoto anapokuwa mtaani hujiingiza kwenye makundi hatarishi.
Ofisa elimu wa shule za msingi katika halmashauri ya Songwe, Michael Nzunda amesema tatizo la utoro sugu kwenye shule za msingi zilizopo katika halmshauri hiyo umetajwa kuwa ni moja ya changamoto inayochangia kushuka kwa kiwango cha elimu wilayani humo na kwamba wanaendelea kuchukua hatua mbalimbali kudhibiti hali hiyo.
Nzunda amesema tayari wamewarejesha shuleni watoto 200 na kwamba wanaendelea kuwafuatilia watoto 1,000 ili waweze kuendelea na masomo.
Ofisa huyo alibainisha sababu tano zinazochangia tatizo la utoro katika halmashauri hiyo kuwa ni shughuli za uchimbaji madini ya dhahabu, ufugaji, uvuvi, umbali wa shule ambapo amesema baadhi ya watoto hutembea umbali wa zaidi ya kilometa 15 kufuta shule.
Philipo Mulugo ambaye ni mbunge wa jimbo la Songwe, alisema amesikitishwa na idadi hiyo ya wanafunzi hao kutofika Shule ambapo amesema atahakikisha anaungana na mkuu wa wilaya katika kukomesha tatizo hilo la utoro kwa halmashauri ya Songwe.
Mashambulizi ya jeshi la Ethiopia Tigary yazuia ngege ya misaada kutua
Mashambulizi ya anga ya jeshi la Ethiopia katika mji mkuu wa jimbo la kaskazini la Tigray, yamesababisha ndege ya misaada ya Umoja wa Mataifa kushindwa kutua mjini Mekelle.
Kwa mujibu wa taarifa ya afisa mratibu wa misaada ya dharura wa Umoja wa Mataifa, Martin Griffths tukio hilo lilitokea jana, Ijumaa na kwamba ndege husika ilirejea mjini Addis Ababa.
Griffths aliongeza kwa kusema tukio hilo linaongeza wasiwasi mkubwa kuhusu usalama wa wafanyakazi wenye dhima ya kutoa misaada ya kiutu katika kusaida raia wenye uhitaji.
Hata hivyo Umoja wa Mataifa ulikuwa na kibali cha safari ya ndege hiyo na haukupata tahadhari ya onyo la mashambulizi ya Makele. Takribani mwaka mmoja tangu kuanza kwa mzozo wa Tigray, kiasi ya watu 400,000 wanakabiliwa na kitisho kikubwa cha njaa, katika eneo hilo la kaskazini mwa Ethiopia.
Hawa Waethiopia wamekula chakula chetu sasa - RPC
Jeshi la Polisi mkoa wa Njombe linawashikilia raia 52 kutoka nchi za Ethiopia na Malawi wanaodaiwa kuingia nchini bila ya kufuata utaratibu wakijaribu kuvuka mipaka kuelekea nchini Afrika Kusini.
Akizungumza mara baada ya kuwakamata raia hao, Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe, Khamis Issah, amesema kuwa watu hao wameharibu tu bajeti ya Taifa, kwani wamekula chakula ambacho hakikuwa kwenye bajeti yao.
Rais wa Burundi awasili visiwani Zanzibar
Na THABIT MADAI, ZANZIBAR
RAIS wa Jamuhuri ya Watu wa Burundi, Jenerali Evariste Ndalishimiye amewasili kwa Mara ya Kwanza Visiwani Zanzibar, Ikiwa ni Muendelezo wa ziara yake ya Siku Tatu Nchini Tanzania.
Mara baada ya kuwasili Visiwani humo Rais Ndalishimiye na Ujumbe wake toka Burundi wamepata fursa ya kuzungumza na Mwenyeji wao Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi, Ikulu Mjini Unguja.
Katika Mazungumzo hayo Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali Mwinyi amempongeza Rais wa Burundi kwa kuhakikisha anasimamia ya Nchi ya Burundi suala la Amani toka aingie madarakani.
“Nikupongeze kwa kuhakikisha kuwa unasimamia suala zima la Amani ya Wananchi wa Burundi toka uingie madarakani,”alisema
Dkt Mwinyi alimueleza kuwa Viongozi wa Tanzania wanaendelea kumuombea katika kuongoza Nchi kwa Amani na Utulivu.
Pia alisema kuwa Zanzibar ni sehemu ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo atahakikisha anaunga mkono harakati za kuimarisha uchumi wa Tanzania na Burundi.
“Nikuhakikishie kuwa naunga mkono jitihada za kuimarisha uchumi wan chi zetu,”alisema.
Kwa upande wake, Rais Jamuhuri ya Burundi Jenerali Evariste Ndalishimiye alipongeza namna Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa namna ya wanavyyonga Nchi kwa kuzingatia msingi ya Utawala bora.
“Sisi kama warundi tunajifunza mengi kutoka Tanzania hivyo niwapongeze hasa Rais Samia Suluhu Hassani kwa namna anavyoiongoza Tanzania,”alieleza.
Katika Hatua nyingine Rais Ndalishimiye, aliishukuru Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwapokea raia Burundi wakati wa machafuko ya wao kwa wao.
Kwa upande wao Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Libarata Mulamula alisema kuwa ziara hiyo imekuja kuongeza ushirikiano baina ya Tanzania na Burundi.
“Ziara hii imekuja kuunganisha sana n asana Tanzania na Burundi,”alisema
Nae Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora Haroun Ali Suleiman amesema kuwa Rais wa Burundi kupitia ziara hiyo amevutika sana kuja kuwekeza Zanzibar katika miradi mbalimbali ya Maendeleo.
Katika Ziara hiyo Rais Evariste Ndalishimiye alipata fursa ya kutembelea miradi mbalimbali ya Maendeleo pamoja na sehemu za kihistoria huku Mwenyeji wake Rais Dkt Mwinyi alimuandalia hafla maalum ya Chakula cha Mchana Ikulu Visiwani Zanzibar.
Ndalichako aagiza kila Mtendaji wa Wizara na Taasisi zitakazotekeleza miradi fedha za UVIKO 19 kukamilisha ifikapo Octoba 30
Na Ezekiel Mtonyole – Dodoma.
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe. Profesa Joyce Ndalichako amewaagiza watendaji wa Wizara na taasisi zitakazotekeleza miradi ya fedha za mpango wa maendeleo kwa ustawi wa taifa na mapambano dhidi ya uvico 19, hadi kufikia Octoba 30, 2021 wawe wamekamilisha mpango na maandalizi ya utelelezaji wa miradi hiyo.
Waziri Prof. Ndalichako ameyabainisha hayo leo Octoba 23, 2021 jijini Dodoma wakati akitoa mchanganuo wa fedha zitakazotekeleza miradi ya fedha hizo miradi ambayo ipo chini ya Wizara ya Elimu ambapo amebainisha kuwa kwa sekta ya Elimu imetengewa bilioni 368.9 na Wizara ya Elimu imepata shilingi bilioni 64.9 kutekeleza miradi iliyochini ya Wizara hiyo.
Ambapo Waziri Ndalichako amesema hadi ifikapo Octoba 30, 2021 kila taasisi itakayotekeleza mradi huo iwe imekamilisha maandalizi na mipango ya utekelezaji ikiwa ni pamoja na kuandaa mpango kazi utakao ainisha hatua mbalimbali za taratibu za manunuzi ya huduma na vifaa.
“Hadi tarehe 30 mwezi huu kila taasisi iwe imekamilisha na iainishe lini vifaa vitanunuliwa, vifaa vyote vinunuliwe kwa kuzingatia bei ya soko nataka na mimi nikienda kununua kifaa bei iwe ndio hiyo” amesema Prof. Ndalichako.
Aidha ameagiza miradi hiyo kuhakikisha inakamilika kabla au ifikapo May 30, 2022 na kusisitiza matokeo ya utekelezaji wa mradi yaendane na thamani ya fedha zilizotolewa na si vinginevyo.
Ameongeza kuwa “Namuagiza Katibu Mkuu wa Wizara aandae mfumo wa uratibu, usimamizi na ufuatiliaji wa miradi utakao wezesha kubaini changamoto zitakazo kuwa zikijitokeza na kuchukua hatua stahiki na kwa wakati” amesema.
Pia ametahadharisha kwamba fedha hizo hazihusishi ulipanaji wa posho ya aina yoyote na viongozi wa taasisi zinazohusika na kwamba yeye atafuatilia kwa ukaribu katika utekelezaji wa miradi hiyo.
Amebainisha kuwa fedha hizo zitakwenda kuimarisha ufundishaji kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu ambapo shilingi bilioni 1.47 zimetengwa, kuimarisha elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stedi ambapo kiasi cha shilingi bilioni 57.98 zimetengwa na kuimarisha mazingira ya utoaji elimu ya ualimu ambapo kiasi cha shilingi bilioni 5.44 zimetengwa.
Urusi na china zimefanya doria ya pamoja katika bahari ya Pasifik
Meli za kivita za Urusi na China zimefanya doria ya kwanza ya pamoja ya kijeshi katika eneo la Magharibi la bahari ya Pasifiki. Ikithibitisha habari hizo wizara ya ulinzi ya Urusi imesema zoezi hilo lilianza Oktoba 17 hadi 23.
Naibu waziri mkuu wa zamani Italia kupandishwa mahakamani kwa kuzuia wahamiaji
Naibu Waziri Mkuu wa Zamani wa Italia, Matteo Salvini leo hii anatarajiwa kupandishwa kizimbani huko katika mji mkuu wa mkoa wa Sicily, Palermo, kutokana na kuhusika kwake na kuizuia meli ya kunusuru wahamiaji kutia nanga katika bandari ya taifa hilo.
UWT kujenga Ofisi zake kwa zaidi ya Sh Milioni 300
UMOJA wa Wanawake Tanzania (UWT) umesema kuwa katika kuiboresha Jumuiya yao na kuifanya kwenda kisasa tayari imeanza ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Dodoma ambazo zitagharimu kiasi cha Sh Milioni 378 Hadi kukamilika kwake.
UWT imesema ujenzi huo umelenga kuifanya Jumuiya hiyo kuondoka katika majengo ya Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambapo kwa sasa ndio wanayotumia kwa shughuli zao na kwamba ujenzi huo utawawezesha kuwa na Ofisi zao wenyewe kwa ajili ya viongozi na watumishi sambamba na ukumbi wa mikutano utakaokua na uwezo wa kubeba watu 200 kwa wakati mmoja.
Akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya UWT kitaifa Wilayani Rufiji mkoani Pwani, Mwenyekiti wa UWT Taifa, Gaudentia Kabaka amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kukubali kuwa mgeni rasmi katika kilele hicho na kwamba yeye ndie Bibi Titi Mohamed mpya wa Tanzania.
Amesema maadhimisho hayo yamefanyika Rufiji kama sehemu pia ya kumuenzi Bibi Titi Mohamed kwa Mchango wake mkubwa katika harakati za kudai Uhuru wa Tanganyika akifanya kazi kwa karibu na Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
" Bibi Titi ndie muasisi wa Jumuiya yetu hii na Mwenyekiti wa kwanza wa UWT Taifa, lakini pia alipata bahati ya kuwa Mbunge wa kwanza mwanamke wa Jimbo hili la Rufiji kwetu sisi ni heshima kusherehekea maadhimisho haya hapa kwake.
Niseme tu kwa sasa tunae Bibi Titi Mohamed mwingine ambaye ni wewe Rais Samia Suluhu Hassan, umeweka rekodi ya kuwa Rais wa kwanza Mwanamke na Mwenyekiti wa Chama chetu, kazi yako iliyotukuka ndani ya miezi michache ya uongozi wako ni kubwa na sisi tuna imani na wewe," Amesema Kabaka.
Awali Katibu Mkuu wa UWT, Dk Philis Nyimbi amesema Jumuiya hiyo itaendelea kushirikiana na Serikali katika kuboresha maisha ya Wanawake nchini ikiwemo kuhakikisha wanajiinua kiuchumi.
Amesema kuelekea maadhimisho ya kilele hicho leo kwa siku ya jana UWT ikiongozwa na Mwenyekiti wake Kabaka ilitembelea maeneo mbalimbali ya kijamii na kutoa mchango wao.
" Jana tulitembelea Shule ya Sekondari ya Utete na kugawa taulo za kike, Hospitali ya Wilaya ya Rufiji ambapo tuligawa mashuka kwa ajili ya wagonjwa sambamba na kituo cha watoto yatima ambao tuliwapelekea mahitaji mbalimbali," Amesema Dk Nyimbi.
Patrice Evra: Mlinzi wa zamani wa Manchester United anasema alinyanyaswa kingono katika umri wa kubalehe
Mchezaji wa zamani wa safu ya ulinzi wa zamani wa Manchester Patrice Evra says anasema alinyanyaswa kingono na mwalimu wake alipokuwa katika umri wa kubalehe.
Evra, mwenye umri wa miaka 40 kwasasa, alizungumzia hilo wazi katika mahojiano na gazeti la The Times la Uingereza kabla ya kutoa kitabu chake.
Alielezea ni kwanini hakuwahi kuzungumzia suala hilo hadi sasa.
"Kwanza nilipoandika kitabu, sikuelezea hadithi yote kwasababu nilikuwa nina aibu na kuogopa ni nini watu wangefikiria ," alisema Evra.
"Sasa ninataka kusema kwasababu sitaki watoto wawe katika hali yangu na kuhisi kuaibika, wakifikiria kwamba hawana ujasiri, inahusuutayari wa akili wa kuzungumzia suala hili.
"Kwahiyio ninataka kuwafanya watoto wawe na ujasiri na wasijilaumu wenyewe, kwasababu kila mara nimekuwa nikijilaumu mwenyewe.
"Sina aibu ya kusema kuwa nilihisi kama muoga kwa miaka mingi kwasababu sikuwahi kuzungumzia unyanyasaji huu wazi.Kilikuwa ni kitu kizito kifuani mwangu.Lakini sikukifanya mwenyewe. Ninafanya kwa ajili ya watoto wengine."
Evra, ambaye alikulia katika kitongoji cha Les Ulis karibu na jiji la Paris, anasema unyanyasaji huo dhidi yake ulifanyika katika nyumba ya mwalimu, ambako aliiishi ili kupunguza muda wa usafiri baina ya nyumbani kwao na shuleni.
Alimwambia tu mama yake wiki mbili zilizopita, na akasema alikataa ombo la mama yake ambaye alimuomba asijadili jambo hilo katika kitabu.
"Ni sasa wakati nina umri wa miaka 40 ndio nimemwambia mama yangu," alisema. "Ulikuwa ni mshituko mkubwa kwake. Alikasirika sana. Aliniambia pole. Alisema, 'Usiweke hili katika kitabu chako, Ni jambo la kibiafsi'.
"Lakini hapo ndipo niliposema, 'Mama, sio kuhusu mimi, ni kuhusu watoto wengine, halafu akaniambia SAWA, anaelewa."
Evra, ambaye alishinda mataji matano ya Primia Ligi katika kipindi cha miaka minane alichokuwa katika Old Trafford,anasema alikanusha unyanyasaji wakati alipopokea simu kutoka kwa polisi kuhusiana na unyanyasaji huo, alipokuwa akichezea klabu ya Monaco akiwa na umri wa miaka 24.
"Kuishi na kumbu kumbu ya unyanyasaji huu ni majuto makubwa sana kwasababu ningekuwa nimewasaidia watu wengi sana ," aliongeza.
Taulo za kike 2500 zatolewa kwa shule za sekondari Rufiji
Oktoba 23, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Gaudentia Kabaka ametembelea Hospitali ya Wilaya ya Rufiji na kukabidhi mashuka 100 sambamba na kukabidhi taulo za kike 2500 kwa Shule ya Sekondari Utete na Ikwiriri.
Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Kabaka amesema UWT ni jumuiya ambayo imekua ikiunga mkono jitihada za Serikali katika sekta mbalimbali hivyo katika kuadhimisha kilele cha wiki yao wameona ni vema wazifikie jamii moja kwa moja.
Kabaka amewataka wanafunzi wa kike kusoma kwa bidii ili kuunga mkono juhudi na jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan ya kuboresha sekta ya elimu na kuwainua wanawake nchini.
Amewaeleza wanafunzi hao umuhimu wa elimu kwa maisha yao ya baadaye.
"UWT Taifa tumefika hapa kuzungumza na nyinyi mabinti wasomi, tumewaletea taulo hizi zipatazo 2500 kwa shule hizi mbili za Ikwiriri na Utete ambazo naamini zitawasaidia kutatua changamoto zenu za kila mwezi za kimaumbile ambazo kwa namna moja ama nyingine huwazuia kuhudhuria masomo yenu.
"Ziepukeni Ndoa za utotoni lakini pia msikubali kupata mimba ili muendelee na elimu na kuweza kufikia malengo yenu, tunaamini ndani ya kundi hili kuna akina Rais Samia wengi, kuna Mwenyekiti wa UWT na mawaziri wengi sana, someni Taifa linawategemea," amesisitiza Kabaka.
Aliyemtumbukiza mtoto wake chooni kuchunguzwa
Jeshi la Polisi mkoani Mbeya, limefanikiwa kumkamata mwanamke Janeth Peter (32), mkazi wa Kiwira wilayani Rungwe kwa tuhuma za kumtupa mtoto wake mwenye umri wa siku tatu ndani ya shimo la choo, ambaye baadaye alikutwa akiwa amefariki dunia.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei, amesema, mtuhumiwa huyo amekamatwa Oktoba 20, 2021 majira ya saa 1:00 usiku baada ya Polisi kufanya msako mkali katika Kata ya Kiwira na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa ambaye amehojiwa na kukiri kutenda kosa hilo.
Matei amesema hadi sasa wanaendelea kumhoji pamoja na uchunguzi wa kitabibu kwa kushirikiana na wataalam wa afya ili kufahamu endapo alitoa mimba au ana matatizo ya kiafya sambamba na kufahamu sababu ya kufanya tukio hilo la kinyama.
Mama amuuza mwanaye kwa Laki 8
Mama huyo anasema amefanya kitendo hicho kwa ajili ya kujisaidia kulipa kodi ya nyumba, kukabiliana na bili zingine kwa kuwa yeye ni maskini.
TAMBUA DALILI ZA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME NA TIBA YAKE, PIA TAMBUA DALILI ZA UGONJWA WA KISUKARI NA TIBA YAKE
Upungufu wa nguvu za kiume ni hali ya kushindwa kufanya tendo kikamilifu shughuli ya tendo la ndoa huhusisha akili,homon,Neva,misuli,hisia na miriji ya damu
DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME
1kuwahi kufika kileleni,2kukosa hamu ya tendo 3kushindwa kurudia tendo la ndoa 4uume kusimama kwa uregevu au kushindwa kusimama 5 kuchoka Sana baada ya tendo la ndoa
TIBA SAHIHI YA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME
Dawa ya MJN ni dawa ya asili isiyokuwa na mkemikali yoyote dawa hii ipo kwenye mfumo wa kunywa na kuchua pia dawa hii ni tamu Sana kwani imechanganywa na asari ni tofauti na ulizowahi kutumia usaidia ata wazee wenye miaka 80 pi uboresha uume wa mwanaume ulioingia ndani na kuwa mfupi
DALILI ZA UGONJWA WA KISUKARI NA TIBA YAKE
1. kunywa maji mengi Sana Kila wakati
2. kwenda haja ndogo Mara kwa Mara
3. kuwa dhaifu ,kukosa nguvu na kijisikia mchovu kila wakati
4. kupunguza uzito au kukonda ata Kama unakula
5. kutoona vizuri
6. mwili kufa gazi hasa miguni
7. vidonda au majeraha sehemu ya mwili kutopona
8 kupungukiwa nguvu za kiume nk
MTN ndio dawa ya kisukari dawa hii inatibu tatizo mojakwamoja endipo ukidhingatia matumizi yake ni dawa isiyokuwa na masharti magumu kwa mtumiaji,pia zipo dawa za vidonda vya tumbo,presha,ngiri,chango la uzazi, miguu kuuma na mgongo nk
WASILIANA NAMI TABIBU DITTU KWA SIMU 0743362017 AU Whatsapp +255714448999 ofisi ipo mbagara sabasaba walio nje ya mkoa utalipia nauri ya mzigo tu sh elfu 12 ukipokea mzigo wako ndio utume pesa
KIWANJA KINAUZWA DODOMA
Tetesi za soka kimataifa
Meneja wa zamani wa Juventus, Chelsea na Inter Milan Antonio Conte "atapenda" kuchukua usuani katika Manchester United iwapo klabu hiyo ya Primia Ligi itamfuta kazi Ole Gunnar Solskjaer. (The Transfer Window Podcast via Star)
Meneja wa zamaniwa Roma Paulo Fonseca, mwenenye umri wa miaka 48, yuko tayari kuteuliwa na Newcastle kama meneja baada ya meneja wa zamani wa Chelsea Frank Lampard kujiondoa katika mbio za kuchukua nafasi ya Steve Bruce katika St James' Park. (Mirror)
Everton wanajiandaa kufanya uhamisho kwa ajili ya mshambuliaji wa Inter Milan na Chile Alexis Sanchez, 32, huku mshambuliaji huyo wa zamani Arsenal na Manchester United akiwa huru kuondoka katika klabu ya Italia katika mwezi wa Januari. (InterLive - in Italian)
Chelsea haitatekeleza azimio lake la awali la kusaini mkataba wa kudumu wa pauni milioni 34 na kiungo wa kati wa Atletico Madrid mwenye umri wa miaka 26, Saul Niguez. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania alihangaika kupata mafanikio ya kimchezo tangu alipojiunga na the Blues kwa mkataba wa mkopo katika mwezi wa Agosti. (La Razon - in Spanish)
Kiungo wa kati wa Manchester United na Uholanzi Donny van de Beek, 24, amemuomba wakala wake kupata uhamisho wake wa kuhamia Real Madrid. (Sun)
Mlinzi Muingereza Chris Smalling, 31, anaweza kuwa mmoja wa wachezaji watakaoondoka Roma katika mwezi wa Julai. (Calciomercato - in Italian)
Mshambuliaji wa Manchester United na Ureno Cristiano Ronaldo, 36, 'aliharibiwa' na 'kuvunja sheria za usawa na unyenyekevu' katika Juventus. (Mail)
Real Madrid Bayern Munich wanaamini kabisa kuwa watasaini mkataba na kiungo wa safu ya kati-nyuma Mjerumani Antonio Rudiger, mweney umri wa miaka 28 ambaye mazungumzo kuhusu mkataba wake na Chelsea yamefikia kiwango cha kukwama. (ESPN)
Mchezaji wa safu ya ulinzi wa kikosi cha vijana wenye chini ya umri wa miaka 21 cha Leicester na Ufaransa Wesley Fofana, 20, anazivutia klabu za Manchester United na Newcastle. (But! Football Club via Sport Witness)
Meneja wa Arsenal Mikel Arteta atakataa ofa yoyote ya kumuuza mshamuliaji Mfaransa Alexandre Lacazette, 30, mwezi Januar, na badala yake atamruhusu kuondoka kwa uhuru wakati mkataba wake utakapoisha katika msimu ujao. (Sun)
Kipaumbele cha Rudiger ni kubakia Chelsea, lakini mchuano wa kutaka saini yake 'uko wazi'. (Fabrizio Romano)
Manchester City, Tottenham, Liverpool na Newcastle zinamtaka winga Mfaransa Ousmane Dembele, 24, ambaye ana uwezekano wa kuondoka Barcelona msimu ujao. (90Min)
Kiungo wa kati wa England Harry Winks, 25, ameleta mashaka juu ya hali yake ya baadaye katika Tottenham baada ya kukiri kwamba amekuwa aking'ang'ana kurejea katika hali yake bora ya zamani ya kimchezo kama sehemu ya mchezaji wa chini ya Nuno Espirito Santo. (Times - subscription required)
Nahodha wa Newcastle na mlinzi Muingereza Jamaal Lascelles, 27, anasema wachezaji lazima wawajibike kwa kufukuzwa kazi kwa Steve Bruce. (Mail)
Manchester City wanajiandaa kujiunga na Barcelona katika mbio za kusaini mkataba na winga Mbrazili mwenye umri wa miaka 21, Antony kutoka klabu ya Ajax. (El Nacional - in Spanish)
West Ham na Southampton wanataka kusaini mkataba na mshambuliaji wa kati wa Sassuolo Mserbia Filip Djuricic, 29, ambaye alicheza nusu ya pili ya msimu wa 2014-15 kwa mkopo katika the Saints. (Calciomercato - in Italian)
Everton wanamtaka kiungo wa Manchester United na England Jesse Lingard, 28, mwezi Januari. (Football Insider)
Kocha wa United Ole Gunnar Solskjaer anasema klabu hiyo haijapokea ofa kutoka Everton kwa ajili ya kiungo wake wa Uholanzi Van de Beek, licha ya uwepo wa tetesi nyingi. (RTL7, via Manchester Evening News)
Umoja wa Mataifa wahofia uhalifu mkubwa kutendeka Myanmar

Umoja wa Mataifa umesema unakhofia janga kubwa zaidi la haki za binaadamu nchini Myanmar, wakati kukiwa na taarifa za maelfu ya wanajeshi wanaolekea kaskazini mwa taifa hilo la kusini mashariki mwa Asia.
"Tunapaswa kuwa tayari kama watu wa eneo hili la Myanmar walivyojitayarisha, kwa uhalifu mkubwa wa halaiki. Ninatamani kwamba niwe siko sahihi," alisema Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa Myanmar, Tom Andrews.
Zaidi ya raia 1,100 wameshauawa kwenye msako mkali dhidi ya wapinzani na wengine zaidi ya 8,000 wametiwa nguvuni tangu mapinduzi hayo, kwa mujibu wa kundi linalofuatilia hali ya mambo nchini Myanmar.
Andrews, ambaye alikuwa akiwasilisha taarifa ya kila mwaka juu ya haki za binaadamu ya Mnyanmar mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, alisema alikuwa amepokea taarifa kwamba makumi kwa maelfu ya wanajeshi wenye silaha nzito walikuwa wanaelekea maeneo ya kaskazini na kaskazini mashariki mwa nchi yaliyo na upinzani mkali.
Uchunguzi uliofanywa, alisema, pia unaonesha kuwa utawala wa kijeshi wa Mnyamar ulikuwa unahusika na matendo ya uhalifu dhidi ya ubinaadamu na uhalifu wa kivita.
"Mbinu hizi zinafanana sana na zile zilizotumiwa na jeshi kabla ya mashambulizi yake ya kimbari dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya katika Jimbo la Rakhine mwaka 2016 na 2017," alisema Andrews.
Kiasi cha Warohingya 740,000 walilikimbia jimbo hilo la Rakhine mwaka 2017 baada ya vikosi vya usalama kuanzisha msako mkali ambao Umoja wa Mataifa umesema ulikuwa sawa na mauaji ya kimbari.
Andrews aliyatolea wito mataifa wanachama kuunyima utawala wa kijeshi wa Myanmar fedha, silaha na uhalali inaoutaka, akitaja kitendo cha kuachiwa kwa baadhi ya wafungwa mapema wiki hii kama ushahidi wa jinsi shinikizo la kimataifa linavyofanya kazi.
Siku ya Jumatatu (18 Oktoba), kiongozi wa kijeshi wa Myanmar, Min Aung Hlaing, alitangaza kuachiwa huru wa zaidi ya watu 5,000 waliokuwa wamefungwa jela kwa kuandamana dhidi ya mapinduzi yake ya kijeshi.
Uamuzi huo ulitangazwa siku chache kabla ya Jumuiya ya Mataifa ya Kusini Mashariki mwa Asia (ASEAN) kutangaza hatua ya kuutenga utawala huo wa kijeshi kabla ya mkutano wa kilele wa mataifa hayo kumi.
"Tangazo la ASEAN kwamba watawala wa kijeshi hawatakaribishwa kwenye mkutano ujao wa kilele lilipiga mahala ndipo," alisema Andrews.
Mjumbe huyo maalum wa Umoja wa Mataifa aliongeza kwamba vikosi vinavyodhibitiwa na jeshi vimewalazimisha watu robo milioni kuyakimbia makaazi yao. Wengi wa hao wamewaji kukamatwa, wakiwemo makumi ya waliopoteza maisha kutokana na mateso.
Andrews alisema amepokea taarifa za uhakika kuwa watoto pia wamekuwa wakiteswa na utawala wa kijeshi wa Myanmar.
Maua Sama anunua gari nyingine
Hakika huu ni mwaka wenye neema kwa Maua Sama kwasababu licha ya ngoma zake kufanya vizuri kupitia digital platforms mbalimbali pia amefanikiwa kulamba madili makubwa ya ubalozi ikiwemo UBALOZI wa TPB Bank.
Maua ambaye hivi karibuni alitangaza kuwa amepona matatizo yaliyokuwa yakimsumbua kwa takribani miezi saba ya kusikia pamoja na kinywa, mbali ya kuwa msanii pia amesomea mambo ya masoko 'marketing'.
Sasa good news ni kwamba tukiwa tunaelekea ukingoni mwa mwaka 2021, Maua Sama ameamua kuvuta ndinga (gari) yake mpya aina ya Toyota Vanguard. Maua ame-share habari hiyo njema na mashabiki wake kupitia ukurasa wake wa instagram.
Kwasasa Maua anakuwa ameongeza listi ya magari yatakayo patikana kwenye parking yake.
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...



