Search This Blog

Saturday, October 23, 2021

Rais wa Burundi awasili visiwani Zanzibar


Na THABIT MADAI, ZANZIBAR

 

RAIS wa Jamuhuri ya Watu wa Burundi, Jenerali Evariste Ndalishimiye amewasili kwa Mara ya Kwanza Visiwani Zanzibar, Ikiwa ni Muendelezo wa ziara yake ya Siku Tatu Nchini Tanzania.

 

Mara baada ya kuwasili Visiwani humo Rais Ndalishimiye na Ujumbe wake toka Burundi wamepata fursa ya kuzungumza na Mwenyeji wao Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi, Ikulu Mjini Unguja.

 

Katika Mazungumzo hayo Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali Mwinyi amempongeza Rais wa Burundi kwa kuhakikisha anasimamia ya Nchi ya Burundi suala la Amani toka aingie madarakani.

 

“Nikupongeze kwa kuhakikisha kuwa unasimamia suala zima la Amani ya Wananchi wa Burundi toka uingie madarakani,”alisema

 

Dkt Mwinyi alimueleza kuwa Viongozi wa Tanzania wanaendelea kumuombea katika kuongoza Nchi kwa Amani na Utulivu.

 

 

Pia alisema kuwa Zanzibar ni sehemu ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo atahakikisha anaunga mkono harakati za kuimarisha uchumi wa Tanzania na Burundi.

 

“Nikuhakikishie kuwa naunga mkono jitihada za kuimarisha uchumi wan chi zetu,”alisema.

 

 

Kwa upande wake, Rais Jamuhuri ya Burundi Jenerali  Evariste Ndalishimiye alipongeza namna Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa namna ya wanavyyonga Nchi kwa kuzingatia msingi ya Utawala bora.

 

 

“Sisi kama warundi tunajifunza mengi kutoka Tanzania hivyo niwapongeze hasa Rais Samia Suluhu Hassani kwa namna anavyoiongoza Tanzania,”alieleza.

 

 

Katika Hatua nyingine Rais Ndalishimiye, aliishukuru Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwapokea raia Burundi wakati wa machafuko ya wao kwa wao.

 

 

Kwa upande wao Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Libarata Mulamula alisema kuwa ziara hiyo imekuja kuongeza ushirikiano baina ya Tanzania na Burundi.

 

“Ziara hii imekuja kuunganisha sana n asana Tanzania na Burundi,”alisema

 

 

Nae Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora Haroun Ali Suleiman amesema kuwa Rais wa Burundi kupitia ziara hiyo amevutika sana kuja kuwekeza Zanzibar katika miradi mbalimbali ya Maendeleo.

 

 

Katika Ziara hiyo Rais Evariste Ndalishimiye alipata fursa ya kutembelea miradi mbalimbali ya Maendeleo pamoja na sehemu za kihistoria huku Mwenyeji wake Rais Dkt Mwinyi alimuandalia hafla maalum ya Chakula cha Mchana Ikulu Visiwani Zanzibar.

 

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...