Search This Blog

Friday, January 31, 2020

USHUHUDA WANGU KWA MBWANA SAMATTA-6 : Haya ndo matarajio pale Aston Villa

By Edo Kumwembe

Hatimaye Samatta alitua Villa na sio Newcastle United. Kabla ya hapo alihusishwa pia kwenda Napoli ambayo ilimuona na kufurahia kiwango chake wakati wa mechi mbili za Ligi ya Mabingwa Ulaya kati ya Genk na Napoli.

Lakini pia Samatta alikuwa na nafasi ya kucheza Ujerumani kwa sababu mawakala wake wanatoka Ujerumani, na wanajuana na mabosi wa timu nyingi za kule. Hata hivyo, ndoto yake kubwa ilikuwa kucheza katika Ligi Kuu ya England.

Kwanini Aston Villa? usajili wa Januari siku zote ni mgumu. Timu huwa zinasajili wachezaji kwa ajili ya kuziba mapengo na upungufu uliojitokeza ndani ya kipindi kifupi tu tangu ligi ianze. Ndani ya miezi mitano tu kuna upungufu unakuwa umejitokeza.

Lakini pia uhamisho wa Januari unategemea zaidi nani anakwenda wapi ili nafasi ipatikane. Kwa mfano, Crystal Palace walimtaka Samatta, lakini hapohapo walikuwa wanasubiri kuona kama wanaweza kumnasa Olivier Giroud kwanza. Kama wakimkosa Giroud ndipo wamchukue Samatta.

Klabu zote za England zilitambua uwezo wa Samatta na zilithibitisha kwamba anaweza kucheza England, hasa baada ya kufunga mabao mawili ya kichwa dhidi ya Liverpool. moja lilikataliwa pale kwao Genk, jingine lilikubaliwa pale Anfield.

Kufa kufaana. Nafasi ya Samatta Villa imepatikana baada ya kuumia kwa Mbrazil Wesley Moraes. Huyu atakuwa nje mpaka mwishoni mwa msimu. Kinachoshangaza ni kwamba Wesley alinunuliwa na Villa akitokea Club Brugge ya Ubelgiji katika dirisha kubwa lililopita huku Samatta akiendelea kusota Genk.

Advertisement

Wesley alikuwa amefunga mabao 16 tu msimu uliopita pale Ubelgiji, lakini ni wazi kwamba kuna mambo matatu yalisababisha achukuliwe na Villa mbele ya Samatta. Kwanza ni Ubrazil wake, pili ni umri wake kuwa chini ya ule wa Samatta, lakini tatu Wesley ni mrefu na umbo lake linaonekana kufaa zaidi kwa Ligi Kuu ya England.

Hata hivyo, kwa nilivyowatazama Wesley pamoja na mshambuliaji wa Newcastle, Joelinton ambaye Newcastle waliamua kumchukua mbele ya Samatta, sioni ambaye ana uwezo mkubwa wa kumshinda Samatta. Lilikuwa suala la muda tu kabla ya Samatta kwenda England Januari. Muda tu.

Kitu kizuri zaidi kwa Samatta katika uhamisho huu ni kwamba mshambuliaji mwingine ambaye alikuwa anasaidiana na Wesley pale Villa, staa wa kimataifa wa Ivory Coast, Jonathan Kodja alikuwa anaonyesha kiwango kibovu na alipanga kuondoka Januari, na tayari ameshaenda Qatar.

Hii ina maana bado Samatta angeenda Villa hata kama Wesley angekuwa na miguu mizima. Nini kinafuata kwa Samatta? Nina uhakika kama atabakia kuwa na afya njema basi ataiteka Ligi kuu ya England bila ya wasiwasi.

Katika ligi hii ambayo inapendelea krosi za juu na chini, Samatta atawaonyesha yeye ni nani. Samatta ni mtaalamu sana wa mipira ya hewani na hapana shaka kwamba atafunga mabao mengi. Alishaonyesha katika mechi mbili za Ulaya dhidi ya Liverpool kwamba soka la England halitamsumbua kufunga mabao.

Kwa sasa ametinga England akiwa na umri wa miaka 27 lakini nampa mwaka mmoja na nusu kuondoka Aston Villa kwenda timu kubwa zaidi. Akiwa na umri wa miaka 27 Samatta bado ana umri sahihi wa kwenda timu kubwa zaidi.

Kuanzia sasa mpaka mwishoni mwa msimu anaweza kufunga mabao sita hadi saba, lakini kuanzia msimu ujao anaweza kufanya mambo makubwa zaidi. Kama Villa isiposhuka na Samatta akaenda katika mazoezi ya maandalizi ya msimu mpya (pre season) anaweza kufanya mambo makubwa zaidi.

Kwa kipindi hiki cha kuanzia sasa mpaka mwishoni mwa msimu atakitumia zaidi kuzoea mazingira. Kuanzia msimu ujao hatakuwa mgeni tena. Atawaonyesha yeye ni nani. Hata Genk ilikuwa hivyo hivyo. Hakuanza kwa kasi ambayo alimaliza nayo.

Katika msimu kamili kama akifunga mabao 15 tu, anaweza kupata dili la kwenda katika timu kama Chelsea, Arsenal, Manchester United na nyinginezo za kariba hiyo. Ni suala la kukimbizana na muda tu na wala sina hofu na Samatta.

Kitu cha msingi katika kikosi cha Villa ni kumlisha mipira tu. Juzi Samatta amecheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Leicester katika pambano la nusu fainali michuano ya Carabao. Villa hawakumlisha vyema kwa sababu walicheza na timu ngumu ambayo iliwatawala. Alipoteza nafasi moja tu ya wazi lakini hakupata nafasi nyingi.

Katika mechi nyingine atapata nafasi nyingi na atafunga mabao mengi. Sio kila kitu ni Leicester. Watakuja akina Bournemouth na watakumbana na makali yake. Kila la heri kwa Mbwana Ally Samatta. Hii ndio safari yake ya kutoka Mbagala mpaka Aston Villa kwa kadri ninavyomfahamu.

Let's block ads! (Why?)

Conte anavyobeba mastaa kuizima Juve Italia

MILAN, ITALIA . CHEKI msimamo wa Serie A unavyosomeka. Juventus ipo kileleni ikiwa imekusanya pointi 51 baada ya mechi 21. Chini yake, kwenye nafasi ya chini ipo Inter Milan, iliyokusanya pointi 48 baada ya kushuka uwanjani mara 21.

Kwenye mechi hizo, Juve imeshinda 16 na Inter 14 huku Juve ikitoka sare mara tatu na kuchapwa mbili, wakati Inter imetoka sare mara sita na kuchapwa mara moja. Timu hizo zimetofautiana pointi tatu tu.
Na Kocha Antonio Conte baada ya kutua tu Inter, kitu chake cha kwanza alichopania ni kumaliza ubabe wa Juventus kwenye kubeba taji la Serie A kwa misimu kibao mfululizo.
Katika kulimaliza hilo, Conte, anayependeleza zaidi kutumia fomesheni ya 3-5-2 amevamia kwenye Ligi Kuu England na kunasa mastaa kadhaa akiamini watakwenda kumaliza ubabe wa Juventus.
"Ukimwondoa Diego Godin, wachezaji wengine wote hawajashinda kitu, hawana uzoefu," alisema Conte.
Katika kuhakikisha anashusha wazoefu kwenye kikosi chake, Conte amevamia kwenye Ligi Kuu England na kwenda kuwanasa mastaa kadhaa ambao mwenye anaamini wakitua katika kikosi chake watakuja kuifanya kuwa ya kiushindani zaidi, ambapo alivamia Manchester United akawanasa mastaa watatu, washambuliaji Romelu Lukaku na Alexis Sanchez (mkopo) kisha akamchukua beki wa pembeni, Ashley Young. Conte amemnasa pia staa mwingine aliyetamba kwenye Ligi Kuu England, Victor Moses, ambaye alikuwa naye huko Chelsea na kwenye dirisha la Januari, amevamia Tottenham Hotspur kwenda kumnyakua kiungo Christian Eriksen.
Na sasa Conte kikosi chake cha kwanza huko Inter akitumia mfumo wa 3-5-2, golini ni Handanovic, atakayelindwa na ukuta wa mabeki watatu, De Vrij, Godin na Young na kwenye kiungo kutakuwa na mastaa watano, Vecino, Eriksen, Sensi, Moses na Sanchez na kwenye fowadi ni Lukaku na Martinez.

Let's block ads! (Why?)

[unable to retrieve full-text content]

[unable to retrieve full-text content]

Guardiola akubali mziki wa Maguire

MANCHESTER, ENGLAND . PEP Guardiola amemwaga sifa kwa mastaa watano wa Manchester United ambao wamemkosha sana kwenye mchezo wa marudiano wa nusu fainali ya Kombe la Ligi ambapo waliichapa timu yake ya Manchester City 1-0 uwanjani Etihad.
Hata hivyo, chama la Guardiola ndilo lililotinga fainali kwa kusonga mbele kwa jumla ya mabao 3-2 baada ya mchezo wa kwanza uliofanyika Old Trafford kuibuka na ushindi wa 3-1. Kwenye fainali itakipiga na Aston Villa uwanjani Wembley.
Na Guardiola anaamini timu yake itacheza vizuri kwenye mchezo huo wa fainali utakaopigwa Machi baada ya kucheza chini ya kiwango dhidi ya Man United.
Baada ya filimbi ya mwisho katika mchezo huo, Guardiola aliyataja majina ya wachezaji watano ambao hakika walimfurahisha kutoka kwenye kikosi cha wapinzani wake, ambao ni Victor Lindelof, Luke Shaw, Harry Maguire, Fred na Nemanja Matic.
"Nimependa namna walivyokuwa wakicheza," alisema Guardiola.
"Old Trafford tulicheza vizuri sisi, pengine sikutarajia hivi tulivyocheza, unaweza kusema kwamba hatukuhitaji sana, lakini ukweli ni kwamba wachezaji wao walikuwa vizuri, walicheza kwa namna ile kocha wao alihitaji wacheze.
"Pengine wanashida tu ya kucheza kwa ubora uleule kila mechi, wanashinda wanapocheza nyumbani, lakini ni timu inayocheza soka safi. Namjua Lindelof nilimwona Benfica, Luke Shaw ni mchezaji mzuri na Maguire ni mmoja kati ya mabeki bora kabisa wa kati duniani."

Let's block ads! (Why?)

Mwimbaji Huyu Atangaza Kuzikata Nyeti zake ili Asahau Kabisa Mambo ya Mapenzi

Pichani Queen Haizel mwimbaji wa Ghana katika interview mpya amewaacha watu midomo wazi kwa kufunguka kuwa kuanzia sasa muda wowote ataziteketeza sehemu zake nyeti ili asahau kabisa issue za mapenzi kusudi ajikite vizuri Kwenye kazi zake za muziki akidai zimekuwa kikwazo kwa maendeleo yake. Amesema ataenda nje ya nchi kwa miezi miwili kufikia lengo hilo la kuzikata

Burna Boy Akutana na Angelique Kidjo Aliyempiga Chini Tuzo za Grammy

Siku 5 baada ya kumalizika tuzo za Grammy, Burna Boy pamoja na Mama yake mzazi wamekutana na Angelique Kidjo ambaye alikuwa mshindi wa kipengele ambacho wengi walimtabiria Burna kushinda. Ila bahati haikuwa kwake
.
But sina uhakika sana kama angelina kidjo alistahiki ile tuzo kwa mwaka 2019/2020 maana wengi wetu wamemjua angerlina kupitia zile tuzo. Kwa maana hakua na kiwango kikubwa cha mziki cha kumshinda burna boy,
.
Na ndio maana hata yy angerlina baada ya kulitambua jambo hilo akaamua kui dedicate ile tuzo kwa burna boy maana hata yy angerlina alijua kabsa kwamba alie deseeve ile tuzo ni burna na yy ilidondoka kwake km bahati mbaya.

BREAKING NEWS: Makonda apigwa marufuku kuingia Marekani


Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imemwekea vikwazo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Christian Makonda kwa madai ya kuhusika katika uvunjifu kamili wa haki za binadamu na tuhuma nyingine. Pia vikwazo hivyo amewekewa mke wake Makonda, Mary Felix Massenge.

Taarifa iliotolewa Ijumaa na wizara ya mambo ya nje ya Marekani imeelezea tuhuma hizo ni uvunjaji wa haki za binadamu, ukandamizaji wa siasa za upinzani, ukandamizaji wa haki ya kujieleza na mikusanyiko, na kuwakandamiza watu ambao wanatengwa katika jamii.

Wizara ya Mambo ya Nje inasema ina taarifa zakuaminika kuwa Makonda alihusika katika uvunjaji wa amani katika nafasi yake kama mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam.

Sheria ya Marekani inaagiza kuwa, katika hali ambayo Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani ana habari za kuaminika kwamba maafisa wa nchi nyingine wamehusika na ufisadi mkubwa au ukiukaji wa haki za binadamu, watu hao na wana familia wa karibu hawataruhusiwa kuingia nchini Marekani.

Marekani inasema ina wasiwasi kwa kuendeleakukosekana uzingatiaji wa haki za binadamu na utawala wa sheria nchini Tanzania.

Hii ni pamoja na hatua ya serikali ya Tanzania inayochukua kukandamiza uhuru wa kujieleza, uhuru wa kujiunga na chama, uhuru wa mikutano ya Amani; kulengwa kwa watu wanaotengwa na vyama vya upinzani vya siasa, na hatarisho la maisha ya watu.

Salim Mtango amtwanga kwa TKO bondia Mthailand katika round ya 7

 

Bondia Salim Mtango amefanikiwa kumtwanga mpinzani wake Suriya Tatakhum kutoka Thailand katika round ya 7.

Pambano hilo limefanyika leo katika kiwanja cha Mkwakwani mkoani Tanga,  Salim Mtango sasa amekuwa ni Bingwa mpya wa Dunia UBO kwa ushindi wa TKO.



JPM Ateua viongozi wengine, Dkt. Abbas awa Katibu Mkuu Wizara ya Habari


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli ameteua viongozi wa taasisi mbalimbali wakiwemo Makatibu Wakuu, viongozi katika majeshi na mahakama.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, leo Januari 31, 2020 Rais Magufuli amemteua Mary Makondo Gasper Makondo kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Bi. Makondo ambaye awali alikuwa Kamishna wa Ardhi amechukua nafasi ya Bi. Doroth Mwanyika ambaye amestaafu.

Aidha, Balozi Kijazi ameeleza kuwa Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Maelezo, Dkt. Hassan Abbas kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo. Amechukua nafasi ya Bi. Suzan Mlawi ambaye pia amestaafu.

Wizara ya Viwanda na Biashara nayo imepata Katibu Mkuu mpya ambaye ni Profesa Riziki Silas Shemdoe ambaye awali alikuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma; akichukua nafasi ya Profesa Joseph Bucheshwaija ambaye amestaafu.

Wengini ni Bi. Zena Ahmed Said (Katibu Mkuu Wizara ya Nishati), Christopher Kadio (Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi), Bw. Leonard R. Masanja (Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati).

Wengine walioteliwa ni kama inavyoonesha sehemu ya Barua ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu:



Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi February 1
















Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi February 1


Guardiola akubali mziki wa Maguire

MANCHESTER, ENGLAND . PEP Guardiola amemwaga sifa kwa mastaa watano wa Manchester United ambao wamemkosha sana kwenye mchezo wa marudiano wa nusu fainali ya Kombe la Ligi ambapo waliichapa timu yake ya Manchester City 1-0 uwanjani Etihad.
Hata hivyo, chama la Guardiola ndilo lililotinga fainali kwa kusonga mbele kwa jumla ya mabao 3-2 baada ya mchezo wa kwanza uliofanyika Old Trafford kuibuka na ushindi wa 3-1. Kwenye fainali itakipiga na Aston Villa uwanjani Wembley.
Na Guardiola anaamini timu yake itacheza vizuri kwenye mchezo huo wa fainali utakaopigwa Machi baada ya kucheza chini ya kiwango dhidi ya Man United.
Baada ya filimbi ya mwisho katika mchezo huo, Guardiola aliyataja majina ya wachezaji watano ambao hakika walimfurahisha kutoka kwenye kikosi cha wapinzani wake, ambao ni Victor Lindelof, Luke Shaw, Harry Maguire, Fred na Nemanja Matic.
"Nimependa namna walivyokuwa wakicheza," alisema Guardiola.
"Old Trafford tulicheza vizuri sisi, pengine sikutarajia hivi tulivyocheza, unaweza kusema kwamba hatukuhitaji sana, lakini ukweli ni kwamba wachezaji wao walikuwa vizuri, walicheza kwa namna ile kocha wao alihitaji wacheze.
"Pengine wanashida tu ya kucheza kwa ubora uleule kila mechi, wanashinda wanapocheza nyumbani, lakini ni timu inayocheza soka safi. Namjua Lindelof nilimwona Benfica, Luke Shaw ni mchezaji mzuri na Maguire ni mmoja kati ya mabeki bora kabisa wa kati duniani."

Let's block ads! (Why?)

Guardiola akubali mziki wa Maguire

MANCHESTER, ENGLAND . PEP Guardiola amemwaga sifa kwa mastaa watano wa Manchester United ambao wamemkosha sana kwenye mchezo wa marudiano wa nusu fainali ya Kombe la Ligi ambapo waliichapa timu yake ya Manchester City 1-0 uwanjani Etihad.
Hata hivyo, chama la Guardiola ndilo lililotinga fainali kwa kusonga mbele kwa jumla ya mabao 3-2 baada ya mchezo wa kwanza uliofanyika Old Trafford kuibuka na ushindi wa 3-1. Kwenye fainali itakipiga na Aston Villa uwanjani Wembley.
Na Guardiola anaamini timu yake itacheza vizuri kwenye mchezo huo wa fainali utakaopigwa Machi baada ya kucheza chini ya kiwango dhidi ya Man United.
Baada ya filimbi ya mwisho katika mchezo huo, Guardiola aliyataja majina ya wachezaji watano ambao hakika walimfurahisha kutoka kwenye kikosi cha wapinzani wake, ambao ni Victor Lindelof, Luke Shaw, Harry Maguire, Fred na Nemanja Matic.
"Nimependa namna walivyokuwa wakicheza," alisema Guardiola.
"Old Trafford tulicheza vizuri sisi, pengine sikutarajia hivi tulivyocheza, unaweza kusema kwamba hatukuhitaji sana, lakini ukweli ni kwamba wachezaji wao walikuwa vizuri, walicheza kwa namna ile kocha wao alihitaji wacheze.
"Pengine wanashida tu ya kucheza kwa ubora uleule kila mechi, wanashinda wanapocheza nyumbani, lakini ni timu inayocheza soka safi. Namjua Lindelof nilimwona Benfica, Luke Shaw ni mchezaji mzuri na Maguire ni mmoja kati ya mabeki bora kabisa wa kati duniani."

Let's block ads! (Why?)

Guardiola akubali mziki wa Maguire

MANCHESTER, ENGLAND . PEP Guardiola amemwaga sifa kwa mastaa watano wa Manchester United ambao wamemkosha sana kwenye mchezo wa marudiano wa nusu fainali ya Kombe la Ligi ambapo waliichapa timu yake ya Manchester City 1-0 uwanjani Etihad.
Hata hivyo, chama la Guardiola ndilo lililotinga fainali kwa kusonga mbele kwa jumla ya mabao 3-2 baada ya mchezo wa kwanza uliofanyika Old Trafford kuibuka na ushindi wa 3-1. Kwenye fainali itakipiga na Aston Villa uwanjani Wembley.
Na Guardiola anaamini timu yake itacheza vizuri kwenye mchezo huo wa fainali utakaopigwa Machi baada ya kucheza chini ya kiwango dhidi ya Man United.
Baada ya filimbi ya mwisho katika mchezo huo, Guardiola aliyataja majina ya wachezaji watano ambao hakika walimfurahisha kutoka kwenye kikosi cha wapinzani wake, ambao ni Victor Lindelof, Luke Shaw, Harry Maguire, Fred na Nemanja Matic.
"Nimependa namna walivyokuwa wakicheza," alisema Guardiola.
"Old Trafford tulicheza vizuri sisi, pengine sikutarajia hivi tulivyocheza, unaweza kusema kwamba hatukuhitaji sana, lakini ukweli ni kwamba wachezaji wao walikuwa vizuri, walicheza kwa namna ile kocha wao alihitaji wacheze.
"Pengine wanashida tu ya kucheza kwa ubora uleule kila mechi, wanashinda wanapocheza nyumbani, lakini ni timu inayocheza soka safi. Namjua Lindelof nilimwona Benfica, Luke Shaw ni mchezaji mzuri na Maguire ni mmoja kati ya mabeki bora kabisa wa kati duniani."

Let's block ads! (Why?)

Guardiola akubali mziki wa Maguire

MANCHESTER, ENGLAND . PEP Guardiola amemwaga sifa kwa mastaa watano wa Manchester United ambao wamemkosha sana kwenye mchezo wa marudiano wa nusu fainali ya Kombe la Ligi ambapo waliichapa timu yake ya Manchester City 1-0 uwanjani Etihad.
Hata hivyo, chama la Guardiola ndilo lililotinga fainali kwa kusonga mbele kwa jumla ya mabao 3-2 baada ya mchezo wa kwanza uliofanyika Old Trafford kuibuka na ushindi wa 3-1. Kwenye fainali itakipiga na Aston Villa uwanjani Wembley.
Na Guardiola anaamini timu yake itacheza vizuri kwenye mchezo huo wa fainali utakaopigwa Machi baada ya kucheza chini ya kiwango dhidi ya Man United.
Baada ya filimbi ya mwisho katika mchezo huo, Guardiola aliyataja majina ya wachezaji watano ambao hakika walimfurahisha kutoka kwenye kikosi cha wapinzani wake, ambao ni Victor Lindelof, Luke Shaw, Harry Maguire, Fred na Nemanja Matic.
"Nimependa namna walivyokuwa wakicheza," alisema Guardiola.
"Old Trafford tulicheza vizuri sisi, pengine sikutarajia hivi tulivyocheza, unaweza kusema kwamba hatukuhitaji sana, lakini ukweli ni kwamba wachezaji wao walikuwa vizuri, walicheza kwa namna ile kocha wao alihitaji wacheze.
"Pengine wanashida tu ya kucheza kwa ubora uleule kila mechi, wanashinda wanapocheza nyumbani, lakini ni timu inayocheza soka safi. Namjua Lindelof nilimwona Benfica, Luke Shaw ni mchezaji mzuri na Maguire ni mmoja kati ya mabeki bora kabisa wa kati duniani."

Let's block ads! (Why?)

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi February 1


















MAGAZETI YA LEO 1/2/2020


















Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...