Search This Blog

Saturday, October 23, 2021

Aliyemtumbukiza mtoto wake chooni kuchunguzwa


Jeshi la Polisi mkoani Mbeya, limefanikiwa kumkamata mwanamke Janeth Peter (32), mkazi wa Kiwira wilayani Rungwe kwa tuhuma za kumtupa mtoto wake mwenye umri wa siku tatu ndani ya shimo la choo, ambaye baadaye alikutwa akiwa amefariki dunia.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei, amesema,  mtuhumiwa huyo amekamatwa Oktoba 20, 2021 majira ya saa 1:00 usiku baada ya Polisi kufanya msako mkali katika Kata ya Kiwira na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa ambaye amehojiwa na kukiri kutenda kosa hilo.

Matei amesema hadi sasa wanaendelea  kumhoji  pamoja na uchunguzi wa kitabibu kwa kushirikiana na wataalam wa afya ili kufahamu endapo alitoa mimba au ana matatizo ya kiafya sambamba na kufahamu sababu ya kufanya tukio hilo la kinyama.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...