Kuelekea maadhimisho ya wiki ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kitaifa leo
Oktoba 23, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Gaudentia Kabaka ametembelea Hospitali ya Wilaya ya Rufiji na kukabidhi mashuka 100 sambamba na kukabidhi taulo za kike 2500 kwa Shule ya Sekondari Utete na Ikwiriri.
Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Kabaka amesema UWT ni jumuiya ambayo imekua ikiunga mkono jitihada za Serikali katika sekta mbalimbali hivyo katika kuadhimisha kilele cha wiki yao wameona ni vema wazifikie jamii moja kwa moja.
Kabaka amewataka wanafunzi wa kike kusoma kwa bidii ili kuunga mkono juhudi na jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan ya kuboresha sekta ya elimu na kuwainua wanawake nchini.
Amewaeleza wanafunzi hao umuhimu wa elimu kwa maisha yao ya baadaye.
"UWT Taifa tumefika hapa kuzungumza na nyinyi mabinti wasomi, tumewaletea taulo hizi zipatazo 2500 kwa shule hizi mbili za Ikwiriri na Utete ambazo naamini zitawasaidia kutatua changamoto zenu za kila mwezi za kimaumbile ambazo kwa namna moja ama nyingine huwazuia kuhudhuria masomo yenu.
"Ziepukeni Ndoa za utotoni lakini pia msikubali kupata mimba ili muendelee na elimu na kuweza kufikia malengo yenu, tunaamini ndani ya kundi hili kuna akina Rais Samia wengi, kuna Mwenyekiti wa UWT na mawaziri wengi sana, someni Taifa linawategemea," amesisitiza Kabaka.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment