Search This Blog

Saturday, October 23, 2021

Mashambulizi ya jeshi la Ethiopia Tigary yazuia ngege ya misaada kutua

 


Mashambulizi ya anga ya jeshi la Ethiopia katika mji mkuu wa jimbo la kaskazini la Tigray, yamesababisha ndege ya misaada ya Umoja wa Mataifa kushindwa kutua mjini Mekelle. 


Kwa mujibu wa taarifa ya afisa mratibu wa misaada ya dharura wa Umoja wa Mataifa, Martin Griffths tukio hilo lilitokea jana, Ijumaa na kwamba ndege husika ilirejea mjini Addis Ababa.


Griffths aliongeza kwa kusema tukio hilo linaongeza wasiwasi mkubwa kuhusu usalama wa wafanyakazi wenye dhima ya kutoa misaada ya kiutu katika kusaida raia wenye uhitaji.


Hata hivyo Umoja wa Mataifa ulikuwa na kibali cha safari ya ndege hiyo na haukupata tahadhari ya onyo la mashambulizi ya Makele. Takribani mwaka mmoja tangu kuanza kwa mzozo wa Tigray, kiasi ya watu 400,000 wanakabiliwa na kitisho kikubwa cha njaa, katika eneo hilo la kaskazini mwa Ethiopia.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...