Watu wapatao tisa wamekufa Oman na Iran hapo jana baada ya Kimbunga Shaheen kupiga katika maeneo ya pwani ya nchi hizo.
Nchini Oman maafisa wamesema watu wawili wamefariki kutokana na maporomoko ya ardhi na mtoto mmoja alifariki katika mafuriko.
Safari zote za ndege zimefutwa au kuahirishwa, kasi ya upepo ilipofikia kilomita 120 kwa saa moja kaskazini mwa pwani ya Oman. Katika mji mkuu Muscat, maji yalijaa na kufunika matairi ya magari, hali iliyopelekea magari mengi kupungua barabarani.
Na kwa upande wa Iran, watu sita walikufa katika bandari ya Chabahar katika jimbo la kusini mashariki mwa Sistan-Baluchestan.
Shirika la habari la IRNA nchini Iran limesema miundombinu, vinu vya umeme na barabara, viliharibiwa na kimbunga Shaheen
No comments:
Post a Comment