Search This Blog
Monday, October 18, 2021
Sukari ya magendo tani 12 zakamatwa Tunduma
Tani 12 za Sukari ya Magendo ambazo zimeingizwa nchini bila kufuata taratibu na sheria zimekamatwa Mpakani Tunduma kwa ushirikiano mkubwa unafanywa na Mamlaka ya Mapato nchini TRA Mkoa wa Songwe na Mbeya.
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Omary Mgumba ameongoza zoezi la kugawa Sukari hiyo katika taasisi mbalimbali za Mkoa wa Songwe katika shule za bweni, shule za Michezo ,Magereza,Kituo cha watoto yatima,Jeshi la Polisi na Jkt Itaka ambapo tani 6 zimegawiwa katika taasisi hizo na zingine tani 6 zimepelekwa Mkoani Mbeya.
Aidha Mkuu wa Mkoa amewataka wafanyabiashara kuachana na biadhara za Magendo kwani kufanya hivyo ni kuendelea kuikosesha serikali mapato.
Wakati huo huo Mgumba ameipongeza TRA kwa kuendelea kufanya kazi kwa ufanisi na kukusanya kodi bila kutumia nguvu pamoja na kuvuka malengo ya ukusanyaji.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment