Search This Blog

Sunday, October 17, 2021

Maelfu waandamana kudai tume huru ya uchaguzi DRC

 


Polisi nchini Jamuhuri ya Kidemkrasia ya Congo wamefyatua vitoa machozi wakati wanaharakati wa chama tawala walipojaribu kuwazuia maelfu ya wanachama wa upinzani walioandamana wakidai tume huru ya uchaguzi. 

Waandamanaji wa upinzani waliangusha sanamu ya rais Felix Tshisekedi pamoja na bendera ya chama chake cha Union for Democracy and Social Progress UDPS. 

Wanachama wa UDPS walijaribu kuwazuia waandamanaji na polisi wakayatua vitoa machozi ili kuwatawanya kuruhusu maandamano kuendelea. 

Maandamano hayo yaliongozwa na Martin Fayulu, mgombea wa urais mwaka 2018 pamoja na aliyekuwa waziri mkuu Adolphe Muzito. 

Fayulu ameshtumu utawala wa Tshisekedi akidai kwamba umesababisha umaskini na njaa kwa sababu ya kile alichokitaja kama kujighubika kwenye ufisadi.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...