Rais Xi Jinping wa China amesema nchi yake iko tayari kubadilishana na kuimarisha ushirikiano na mataifa mengine. Xi Jinping amesema hayo kwenye ujumbe wake wa video uliopo kwenye maonyesho ya kibiashara yaliyofunguliwa sambamba na yale ya Dubai ya Expo 2020.
Huku akisisitizia maonyesho hayo kufanyika kwa mara ya kwanza Mashariki ya Kati. Xi amesema chini ya maudhui ya "Muunganiko wa Fikra, Ujenzi wa Mustakabali" mataifa yana fursa ya kushirikiana kifilosofia, mafanikio ya kiuchumi, maendeleo pamoja na kukuza majadiliano na ushirikiano, ili kuonyesha umuhimu wa maonyesho hayo ya Expo.
No comments:
Post a Comment