Search This Blog

Friday, September 24, 2021

Tanzia: Mwandishi wa Habari wa ITV amefariki dunia kwa ajali


Mwandishi wa Habari wa ITV na Radio One mkoani Songwe Gabriel Kandonga, amefariki dunia kwa ajali ya gari.

Ajali hiyo imetokea alfajiri ya leo Septemba 24, 2021, wakati akitokea nyumbani kwake Mpemba kuelekea wilayani Songwe katika majukumu yake ya kila siku.

Mkuu wa mkoa wa Songwe Omary Mgumba, amethibitisha kutokea kwa kifo cha mwandishi huyo na kusema ajali hiyo imetokea katika eneo la shule ya Sekondari Mlowo ambapo alikuwa anajaribu kulipita lori na hatimaye kulivaa fuso kwa upande wa nyuma.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...