Dada mwenye ushawishi mkubwa wa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un anasema wako tayari kuanza tena mazungumzo na Korea Kusini ikiwa itamaliza "sera zake za uhasama".
Kim Yo-jong alikuwa akijibu mwito mpya kutoka Korea Kusini kutangaza rasmi kumaliza Vita vya Korea.
Mgogoro huo, ambao uligawanya peninsula hiyo kuwa nchi mbili, ulimalizika mnamo 1953 lakini mkataba wa amani uliosainiwa.
Nchi hizo mbili zimekuwa kwenye vita tangu wakati huo, na zimekumbwa katika uhusiano wenye taharuki wakati mwingine .
Wiki hii, rais wa Korea Kusini Moon Jae-in alitaka Korea mbili na washirika wao – Marekani ambayo inaunga mkono Kusini, na China ambayo ni mshirika mkubwa wa uchumi wa Kaskazini - kutangaza kumaliza mzozo rasmi na kuleta amani katika peninsula hiyo ya Korea .
Wazo hilo hapo awali lilitupiliwa mbali na waziri wa ngazi ya juu wa Korea Kaskazini kama "mapema".
Lakini katika taarifa isiyotarajiwa iliyotolewa Ijumaa kupitia vyombo vya habari vya serikali, Bi Kim alisema wazo hilo lilikuwa "la kupendeza".
Walakini ameongeza kuwa Korea Kaskazini itakuwa tayari tu kujadili pendekezo hilo ikiwa Korea Kusini itaacha kile alichokiita "sera za uhasama" kwao.
"Kinachohitaji kutupiliwa mbali ni mitazamo ya kinafiki , ubaguzi, tabia mbaya na msimamo wa uhasama wa kuhalalisha matendo yao wenyewe huku wakikosoa utekelezaji wetu wa haki ya kujilinda," alisema katika taarifa.
"Ni wakati tu sharti kama hilo litakapotimizwa, itawezekana kukaa uso kwa uso na kutangaza kukomesha vita."

No comments:
Post a Comment