Search This Blog

Saturday, September 25, 2021

Simba, Yanga kumaliza ubishi leo kwa Mkapa


LEO Septemba 25 Uwanja wa Mkapa kunatarajiwa kuwa na mchezo wa kukata na shoka kati ya Simba v Yanga ambao ni wa Ngao ya Jamii.

 Mchezo huo ambao utakuwa ni wa ufunguzi wa msimu mpya wa Ligi Kuu Bara baada ya kumalizika kwa kipindi cha usajili na maandalizi ya msimu mpya unaotarajia kuanza Septemba 27.

Rekodi inaonyesha kwa mwaka huu Yanga na Simba hadi kufikia kwenye mchezo huo zitakuwa zimekutana mara tano katika mashindano yote.

Lakini katika mchezo huo wa Ngao ya Jamii umeanza kuzungumzwa kwa muda na mashabiki wa timu hizo kutokana na uwepo wa wachezaji wengi wapya ambao watakuwa wageni kwenye mchezo huo kwani ni mara yao kwanza kucheza mchezo wa dabi ambao ni mkubwa kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati.





No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...