Search This Blog

Saturday, September 25, 2021

Lowassa ampongeza Rais Samia kwa hotuba Baraza Kuu UN


Waziri Mkuu wa Zamani, Edward Lowassa amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa hotuba yake katika Mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kusema kiongozi huyo amefanikiwa kulirejesha taifa katika ramani ya dunia.

Katika Taarifa yake aliyoitoa hivi punde, Lowassa amempongeza na kumshukuru Rais Samia kwa kuifanya vyema kazi ya kuijenga nchi na kisha kuendeleza safari ya kujenga uchumi imara.

“Kupitia hotuba yake katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, New York Marekani jana Alhamisi, Mama Samia amelirejesha tena taifa letu katika ramani ya dunia,” Lowassa.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...