Search This Blog

Thursday, September 16, 2021

Biashara United kucheza bila mashabiki



Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limekataa maombi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuruhusu washabiki kwenye mechi kati ya Biashara United na FC Dikhil ya Djibouti.

Mechi hiyo ya marudiano ya Kombe la Shirikisho la CAF itachezwa Jumamosi, Septemba 18 mwaka huu saa 1 kamili jioni Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

CAF imesisitiza kuwa mechi zake zote zitachezwa bila washabiki kama ilivyoainishwa katika mwongozo wake na ule wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kuhusu ugonjwa wa Covid-19.


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...