Waziri mkuu wa zamani wa Mali Boubèye Maïga amekamatwa kwa madai ya rushwa katika matumizi ya ndege ya rais miaka saba iliyopita.
Wakili wake Kassoum Tapo alisema taarifa juu ya kukamatwa kwake Alhamisi hii bado haijawekwa wazi.
Bwana Maïga amekuwa akishutumiwa kwa madai ya kuongeza gharama ya malipo ya ndege ya Rais wa zamani Ibrahim Keïta.
Alikuwa waziri wa ulinzi wakati akifanya gharama hizo mwaka 2014.
Ndege hiyo ya rais ilinunuliwa kwa dola milioni 40 (£29m), kiwango cha fedha ambacho kilikosolewa vikali kuwa ni gharama kubwa sana.
Bwana Maïga alikuwa waziri mkuu kati ya mwaka 2017 na 2019 wakati alipojiuzuru baada ya kuibuka kwa ghasia nchini kwake.
Boubou Cissé alichukua wadhifa huo wakati alipoondolewa madarakani pamoja na Rais Keïta mnamo Agosti 2020.

No comments:
Post a Comment