Moto mkubwa zaidi umetokea katika maeneo ya milima katika mkoa wa Kabylie , ambapo wanajeshi 25 wamefariki wakati wakipambana kuzima moto huo.
Rais wa Algeria, Abdelmajid Tebboune ametuma salamu za rambirambi kwa familia za wahanga , amesema wanajeshi wameweza kuwaokoa watu zaidi ya 100 kutoka kwenye moto.
Waziri wa mambo ya ndani anawashuku kuwa wachomaji misitu wanahusika na janga hilo la moto.
Matukio ya moto katika eneo la pori katika mataifa ya ukanda wa Mediterranea yamezidi kutokana na joto kuongezeka na kiwango cha ukame kuongezeka.
Mji mkuu wa Tunisia, Tunis, umeshuhudia kiwango cha juu zaidi cha joto cha nyuzi joto 48C siku ya Jumanne.

No comments:
Post a Comment