Search This Blog

Wednesday, August 11, 2021

Rais wa Afrika Kusini Ramaphosa kufika mbele ya jopo la uchunguzi wa madai ya ufisadi dhidi ya mtangulizi wake Zuma

 


Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa leo anatarajiwa kufika mbele ya jopo la uchunguzi wa madai ya ufisadi dhidi ya mtangulizi wake Jacob Zuma.

Jopo hilo lilianzishwa kuchunguza madai kwamba mtangulizi wake Jacob Zuma - wakati wa kipindi chake uongozini - aliruhusu familia tajiri ya Gupta kupora rasilimali za serikali na kushawishi seraza serikali na uteuzi wa baraza la mawaziri.

Wote wawili Zuma na Gupta wanakanusha makosa yoyote.

Ufisadi huo unakadiriwa kugharimu Afrika Kusini $ 81bn (£ 58bn) fedha za umma na kupoteza fursa nyingi ambazo zingekuwa na manufaa kwa nchi.

Bwana Ramaphosa alikuwa naibu kiongozi wa chama kinachotawala ANC wakati huo.

Ameitwa kujibu maswali juu ya kile chama kilijua, ikiwa kuna chochote, juu ya madai ya utovu wa nidhamu na ikiwa walifanya chochote kujaribu kuzuia uharibifu huo.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...