Search This Blog
Monday, August 23, 2021
Mwenge wasisitiza utunzaji wa mazingira
Utunzaji wa mazingira unapaswa kupewa kiupaumbele hasa kwenye vyanzo vya maji ili kuweza kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi.
Hayo yamesemwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi alipotembelea utunzaji wa chanzo cha maji cha mto Kizinga na kupanda mti katika chanzo hicho kilichoanza mwaka 1950 ambacho kina uwezo wa kuzalisha maji kiasi cha lita milioni 7 hadi 9 kwa siku.
Amesema Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kwa kushirikiana na wananchi wanapaswa kuwa walinzi bora kwenye kulinda vyanzo vya maji, kwani vyanzo vikikauka hakutakuwa na haja ya kuwepo kwa mamlaka hiyo.
Ameongeza kuwa Mwenge wa Uhuru mwaka 2021 umetembelea chanzo hicho kuona uwezo wake wa uzalishaji wa maji pamoja na kuhamasisha upandaji wa miti kwenye vyanzo mbalimbali vya maji.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment