Search This Blog

Monday, August 23, 2021

Azam FC leo wamekwea pipa kuweka kambi Zambia


BAADA ya kukamulisha ishu ya usajili, utambulisho wa nembo mpya, utambulisho wa uzi mpya pamoja na slogan mpya Azam FC leo wamekwea pipa kuelekea Zambia.

Ni Edward Manyama aliyekuwa anakipiga ndani ya Ruvu Shooting ambaye ni nyota pia ndani ya timu ya taifa ya Tanzania,  taifa Stars ni miongoni mwa waliotambulishwa.

Nembo yao mpya ilizinduliwa na mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Habari,  Innocent Bashungwa ambaye alikiri kwamba ni nembo bora.

Kwa upande wa slogan mpya wanakwenda na mwendo wa kimyakimya. Leo wamekwea pipa kuibukia Zambia.

Kwa mujibu wa Mtendaji Mkuu wa Azam FC,  Abdulkalim Amin amesema kuwa watakuwa na maandalizi mazuri yatakayowafanya wapate matokeo chanya.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...