Search This Blog

Monday, August 9, 2021

Jeshi la Indonesia ladokeza kukomesha ‘vipimo vya ubikira’ kwa wanawake wanaojiunga na jeshi


 

Jeshi la Indonesia limedokeza kuwa litakomesha vipimo vya lazima vya "ubikira" kwa makurutu wa kike, katika hatua ambayo imepokelewa vyema na vikundi vya haki za binadamu.

Kwa miongo kadhaa, jeshi limekuwa likiwatakamakurutu wa kike kukubali kupimwa ili kujua iwapo ni mabikira au la ,mtindo ambaokundi la kutetea haki za binadamuHuman Rights watch limesema ni‘dhalilishi’ na ‘usiokuwa na msingi wa kisayansi’

Wakati wa vipimo hivyo , wanawake waliingiziwa vidol viwili katika sehemu zao za siri na daktari wa jinsia yoyote kwa lengo la kujua iwapo walikuwa mabikira au la .

Shirika la HumanRights Watch limesema kitendo hicho ni sawa na "unyanyasaji wa kijinsia."

Upimaji wa ubikira ni kitendo kilichopuuzwa na kulaaniwa ambacho Shirika la Afya Ulimwenguni limesema "halina uhalali wa kisayansi" na ni "ukiukaji wa haki za binadamu za mwathiriwa."

Akizungumza katikahotuba iliyowekwa Youtube mwezi jana mkuu wa jeshijenerali Andika Perkasa aliashiria kwamba vipimo vya ubikira sasa vitakomeshwa na badala yake mafunzo yataangazia ‘uwezo’



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...