Iran imesema iko tayari kufufua mazungumzo ya makubaliano ya nyuklia pamoja na mataifa yenye nguvu ulimwenguni chini ya uongozi wa rais mpya Ebrahim Raisi.
Halikadhalika maafisa wa Umoja wa Ulaya wamesema kwamba mazungumzo yanaweza kuanza mwanzoni mwa mwezi Septemba mjini Vienna, Austria.
Afisa anaetarajiwa kusimamia mazungumzo hayo kwa upande wa Umoja wa Ulaya Enrique Mora, alihudhuria kuapishwa kwa Raisi mjini Tehran siku ya Alhamisi.
Akiwa huko alizungumza na afisa wa Iran aliyeteuliwa kusimamia mazungumzo ya nyuklia, Hossein Amir-Abdollahian.
Aidha kuna fununu kwamba huenda Amir-Abdollahian akateuliwa kama waziri mpya wa mambo ya nje kwenye baraza la mawaziri la Raisi.

No comments:
Post a Comment