Watu 2 walikamatwa kwenye uwanja wa ndege wa Toronto nchini Canada, wakijaribu kuingia nchini na chanjo bandia na nyaraka za vipimo vya corona (Kovid-19).
Katika taarifa iliyotolewa kwenye wavuti rasmi ya Wakala wa Afya ya Umma wa Canada, ilitangazwa kuwa tukio hilo liligunduliwa katika hati ya vipimo na chanjo ya Kovid -19 ya abiria 2 wanaotoka Marekani (USA).
Katika taarifa hiyo, ilibainika kuwa raia 2 wa Canada, ambao majina yao hayakutajwa, walitozwa faini ya dola 19,720 za Canada kila mmoja.
Canada, iliyochukuwa uamuzi wake mnamo Julai 5, ilianzisha kanuni mpya kwa wasafiri wa kimataifa.
Kufuatia kanuni hiyo, kila mtu ambaye anataka kuingia nchini analazimika kuwasilisha hati inayoonyesha kuwa wamepata chanjo zao za Kovid-19.
Wale ambao hawajachanjwa lazima wafanye vipimo vingi na kukaa siku 3 katika hoteli iliyochaguliwa na serikali kabla ya kutengwa kwa siku 14.
Huko Canada, wale wanaokiuka masharti ya Sheria ya Karantini wanaweza kuhukumiwa kifungo cha miezi 6 gerezani au kutozwa faini ya hadi dola elfu 750.
Canada itaanza kuruhusu raia wa Marekani waliopewa chanjo kamili kuingia nchini kuanzia Agosti 9. Walakini, mpaka wa Marekani na Canada na Mexico utabaki kufungwa kwa raia wa kigeni hadi Agosti 21.
No comments:
Post a Comment