Search This Blog
Wednesday, August 4, 2021
Amuua na mwenzake kisa pombe
Jeshi la Polisi Mkoani Kilimanjaro linamshikilia mtu mmoja (jina linahifadhiwa) kwa tuhuma za mauaji ya dereva wa bodaboda aliyefahamika kwa jina la Oscar Kiondo, mkazi wa Kijiji cha Holili wilayani Rombo.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amesema tukio hilo limetokea katika baa ya Afrikasana wilayani humo ambapo mtuhumiwa alimchoma Oscar kwa kitu chenye ncha kali na kusababisha kifo chake.
Kamanda Maigwa amesema chanzo cha ugomvi huo ni ulevi wa pombe kati ya marehemu na mtuhumiwa wakiwa wanakunywa pombe kwenye baa hiyo.
Amesema marehemu Oscar amefariki dunia akiwa njiani kuelekea hospitali ambapo mwili wake umehifadhiwa Hospitali ya Faraja iliyoko kagika Mji Mdogo wa Himo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
No comments:
Post a Comment