Khalid al-Mishri alichaguliwa tena kama Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Kitaifa la Libya.
Kufuatia uteuzi huu, Mishri ameweza kuchaguliwa kuhudumu kwenye wadhifa huu kwa mara ya nne.
Msemaji wa Baraza Kuu la Kitaifa Mohammed en-Nasser alisema kuwa katika duru ya pili ya uchaguzi uliofanyika katika mji mkuu Tripoli, Mishri alishinda kura za wanachama 73 kati ya wajumbe 128, na kumuacha nyuma mpinzani wake Salah Mitu.
Katika taarifa aliyotoa kwa waandishi wa habari baada ya uchaguzi, Mishri alisema,
"Baraza kama taasisi linahitaji kufanya kazi kwa roho ya udugu na natumai kila mtu ataelewa somo lililofundishwa na Baraza leo."
Mishri, ambaye alichaguliwa kwanza kuwa mwenyekiti wa Baraza Kuu la Kitaifa la Libya mnamo Aprili 2018, aliteuliwa kwa nafasi hii kwa mara ya pili mnamo 2019 na kwa mara ya tatu mnamo 2020.

No comments:
Post a Comment