Search This Blog

Wednesday, July 7, 2021

Zimbabwe yatoa noti ya thamani ya juu zaidi


Kuanzia Jumatano nchini Zimbabwe itasambazwa noti mpya ya dola 50, ikiwa ndio yenye thamani kubwa zaidi kuwahi kutolea Zimbabwe tangu mwaka 2019.

Dola 50 ya Zimbabwe ina thamani ya dola $0.60.

Noti mpya ilizunduliwa Jumanne na benki kuu ilisema kuwa itasambaza dola milioni 360 za Zimbabwe kupitia benki.

Imetolewa huku nchi hiyo ikikabiliwa na mfumuko wa bei ambao umewafanya watu kutembea lundo la noti.

Noti mpya ina picha ya shujaa wa kupambana na ukoloni Mbuya Nehanda.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...