Search This Blog
Tuesday, July 27, 2021
Simbachawene aagiza Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kufanya ukaguzi katika shule zote nchini
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene ameliagiza Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kufanya ukaguzi katika shule zote nchini, ili kubaini iwapo kuna vihatarishi vinavyoweza kuwa vyanzo vya moto.
Simbachawene ametoa agizo hilo mkoani Arusha wakati akitembelea baadhi ya maeneo ya taasisi zilizo chini ya wizara anayoiongoza, ikiwa ni hatua za kudhibiti matukio ya shule kuungua moto ambayo yamekuwa yakihatarisha maisha ya wanafunzi na kuharibu mali zao na za shule.
Pia amelisisitiza jeshi hilo kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika visima vya maji ya Zimamoto, na kuhakikisha wapo tayari kukabiliana na ajali za moto muda wowote zinapotokea.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment