Search This Blog

Tuesday, July 27, 2021

Simbachawene aagiza Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kufanya ukaguzi katika shule zote nchini


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene ameliagiza Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kufanya ukaguzi katika shule zote nchini, ili kubaini iwapo kuna vihatarishi vinavyoweza kuwa vyanzo vya moto.

Simbachawene ametoa agizo hilo mkoani Arusha wakati akitembelea baadhi ya maeneo ya taasisi zilizo chini ya wizara anayoiongoza, ikiwa ni hatua za kudhibiti matukio ya shule kuungua moto ambayo yamekuwa yakihatarisha maisha ya wanafunzi na kuharibu mali zao na za shule.

Pia amelisisitiza jeshi hilo kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika visima vya maji ya Zimamoto, na kuhakikisha wapo tayari kukabiliana na ajali za moto muda wowote zinapotokea.


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...