Uchina imeionya Uingereza kuhusu kundi la meli zake za kivita zinazokaribia katika bahari ya Kusini mwa China dhidi ya "vitendo vyovyote visivyofaa " wakati inaingia katika eneo hilo linalozozaniwa .
Msafara wa meli hizo unaongozwa na meli ya kubeba ndege za kivita ya HMS Queen Elizabeth.
'Jeshi la Wanamaji la Ukombozi wa Watu liko katika hali ya juu ya utayari wa mapigano' linasema jarida la Global Times, linaloonekana kutumiwa kutoa kauli za Chama tawala cha Kikomunisti cha China (CCP).
China imekuwa ikifuatilia kwa karibu kinachofanyika katika safari ya msafara huo unaelekea upande wa mashariki kwenda Japan.
Nchi hiyo imeishtumu Uingereza kwa kuendelea kuishi katika 'siku zake za ukoloni".
Jeshi la Wanamaji la Uingereza limekuwa likifanya mazoezi na jeshi la wanamaji la Singapore na Katibu wa Ulinzi wa Uingereza Ben Wallace ameonyesha wazi nia ya kuenelea kufanya mazoezi ya "Uhuru wa kusafiri baharini " kupitia Bahari ya Kusini mwa China.
Kinyume na uamuzi wa korti ya kimataifa ya 2016, China inadai sehemu kubwa ya bahari hiyo kuwa yake na imekuwa ikijishughulisha na kujenga visiwa bandia na njia za kuwezesha ndege kupa , zingine zikiwa karibu na maji ya eneo la nchi jirani.
Meli za kivita za Marekani na Uingereza zimepinga madai ya Uchina juu ya kumiliki Bahari ya Kusini mwa China kwa kuipitia katika bahari hiyo kwa makusudi.

No comments:
Post a Comment