Search This Blog

Tuesday, July 27, 2021

Afisa Elimu wilaya ya Babati afaridi dunia kwa ajali


Na John Walter-Babati
Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari (Afisa elimu) wilaya ya Babati Paulina Mpare, amefariki dunia kwa ajali ya gari baada ya gari alilokuwa anasafiria kupasuka tairi na kuacha njia eneo la Makutupora mkoani Dodoma.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Babati John Nchimbi amethibitisha kifo hicho na kueleza kuwa Mpare alikuwa akirudi Babati akitokea Dar es Salaam alipokuwa akimuuguza ndugu yake.
Nchimbi amesema taarifa alizozipata kutoka kwa wasamaria wema zinaeleza kuwa afisa huyo alifariki dunia julai 26 majira ya jioni akiwa mapokezi katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma alipofikishwa ili kuokoa uhai wake.
'Alipatiwa msaada na wasamaria wema katika gari kampuni ya Shabiby' alieleza Nchimbi
Amesema Mpare alikuwa ni kiungo muhimu katika ukuaji wa taaluma katika Halmashauri ya wilaya.
Kuhusu taratibu za mazishi,Nchimbi amesema wanasubiri utaratibu wa familia.
Kwenye picha ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Babati John Nchimbi






No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...