Virusi aina ya "Delta" vya corona (Covid-19) ambayo viligundulika India kwa mara ya kwanza, vilionekana Palestina.
Waziri wa Afya Mey Keyle alitangaza kwamba virusi aina ya Delta vilionekana kwa wanawake wawili katika Ukingo wa Magharibi uliokaliwa kinyume cha sheria.
Keyle alisema kuwa wanawake hao waliokutwa na maambukizi walikuwa wamerudi hivi karibuni kutoka Falme za Kiarabu (UAE).
Akibainisha kuwa uchunguzi umeanzishwa ili kuwatenga watu waliojumuika na wanawake hao wenye virusi aina ya Delta, Keyle aliwaomba Wapalestina wasisafiri nje ya nchi isipokuwa nyakati za dharura au kukiwa na ulazima.

No comments:
Post a Comment