Baada ya ajali ya basi la Kampuni ya Classic iliyotokea hapo juzi eneo la Didia Wilayani Shinyanga na kusababisha vifo vya watu wanne wakiwemo wanafunzi watatu wa Chuo Kikuu Bugema Jijini Kampala, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Khamis Hamza Chilo ametembelea eneo la tukio sambamba na kuwajulia hali majeruhi waliolazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga kisha akawataka waendesha vyombo vya moto kuwa waangalifu wawapo barabarani.
Aidha kwa upande wake kamanda wa Polisi Mkoani Shinyanga akizungumza juu ya hatua zilizochukuliwa hadi sasa baada ya dereva wa basi hilo kukimbia, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Debora Magiligimba amesema kuwa tayari mtuhumiwa huyo amekatwa wilayani Nzega mkoani Tabora
No comments:
Post a Comment