Wanamgambo 10 wa kundi la Boko Haram waliangamizwa katika operesheni dhidi yao iliyotekelezwa nchini Nigeria.
Msemaji wa jeshi Mohammed Yerima alisema katika taarifa kwamba jeshi lilizuia jaribio la shambulizi la Boko Haram katika mkoa wa Rann, jimbo la Borno.
Akibainisha kuwa magaidi 10 waliuawa katika operesheni dhidi ya Boko Haram baada ya kuzuia shambulizi hilo, Yerima alisema kuwa magaidi wengi walikimbia wakiwa wamejeruhiwa.
Yerima pia alisema kuwa silaha na idadi kubwa ya risasi pamoja na mali za magaidi zilikamatwa.

No comments:
Post a Comment