Waandishi wa habari 3 wa kigeni wameripotiwa kupotea baada ya shambulizi kutekelezwa nchini Burkina Faso.
Katika taarifa zilizotolewa kwenye vyombo vya habari vya kitaifa, iliarifiwa kuwa watu 3 walijeruhiwa na waandishi wa habari 3 wa kigeni pamoja na mwanajeshi walipotea katika shambulizi lililotekelezwa na genge la majangili katika mkoa wa Gurma mashariki mwa nchi.
Ilibainika kwamba waandishi wa habari 3, wawili wakiwa ni raia wa Uhispania na mmoja wa Ireland, huenda walitekwa nyara na washambuliaji.
Maafisa waliripoti kwamba vikosi vya usalama vilipelekwa katika eneo hilo ili kuwatafuta waandishi wa habari na mwanajeshi wa Burkina Faso.
Burkina Faso imekuwa eneo la mashambulizi ya kigaidi tangu 2015. Kutokana na mashambulizi yanayolenga raia na wanajeshi, maelfu ya watu walilazimika kuhamia maeneo salama. Katika mikoa mingine, ilani ya hali ya dharura pia ilitangazwa.

No comments:
Post a Comment