Jeshi la wanamaji la Urusi limeanza zoezi la kijeshi katika Bahari Nyeusi kabla ya meli za kivita za Marekani (USA) kwenda kanda hiyo.
Kulingana na taarifa za mashirika ya habari, meli kutoka Bahari Nyeusi ya kanda ya Urusi huko Crimea, helikopta na ndege zinashiriki katika zoezi hilo.
Katika zoezi hilo, majaribio ya makombora yatatekelezwa kwa kulenga shabaha za ardhini na angani.
Marekani ilitangaza kwamba imetuma meli mbili za kivita katika kanda hiyo ili kukita kambi katika Bahari Nyeusi.
Hatua hiyo iliibuka baada ya Urusi kutuma wanajeshi kwenye mpaka wa Ukraine.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergey Ryabkov, alielezea hatua ya meli za kivita za Marekani kupelekwa kwenye Bahari Nyeusi kuwa kama "uchochezi".

No comments:
Post a Comment