Rais wa Iran Hassan Rouhani alisema kuwa "bado hawajaona nia njema wala mtazamo tofauti" kutoka kwa utawala wa Joe Biden nchini Marekani.
Rouhani, ambaye alihudhuria hafla ya ufunguzi wa miradi ya afya iliyofanyika katika mikoa mbalimbali ya Iran kupitia mkutano wa video, alikosoa utawala wa Marekani katika hotuba yake na kuutaka uchukue hatua juu ya makubaliano ya nyuklia.
Akielezea Donald Trump, ambaye muda wake umemalizika nchini Marekani kuwa kama "gaidi mkubwa aliyekosa heshima", Rouhani alimtaka Biden arejee kwenye njia inayostahili na kusema,
"Sera ya shinikizo kubwa dhidi ya Iran imeshindwa, hakuna mtu ulimwenguni aliye na wasiwasi wowote juu ya suala hili. Bado hatujaona nia njema wala mtazamo tofauti kutoka kwa utawala mpya wa Marekani. Maneno yao yamebadilika, lakini tunapaswa kuona mabadiliko kwa vitendo. Bado haijulikani ni jinsi gani wanataka kufidia mauaji yaliyotekelezwa."
Akibaini kuwa shida zinazowakabili watu wa Iran zinaendelea kwa sababu ya vikwazo vilivyorudishwa na Trump, Rouhani alisema,
"Ikiwa ni mkweli katika mazungumzo yake mapya ya serikali ya Marekani, basi ni lazima abadilishe mwelekeo wake bila kupoteza muda na kufidia yaliyotokea haraka iwezekanavyo."

No comments:
Post a Comment