Kyaw Tint Swe ambaye ni mwanachama wa baraza la mawaziri la serikali iliyoondolewa madarakani baada ya mapinduzi ya kijeshi nchini Myanmar, ameripotiwa kukamatwa.
Katika taarifa iliyotolewa na Chama cha Kitaifa cha Kidemokrasia (NLD) kinachoongozwa na Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje na kiongozi halali wa nchi Aung San Suu Kyi, iliripotiwa kuwa Swe, ambaye alikuwa kwenye baraza la mawaziri katika Serikali ya Suu Kyi alizuiliwa usiku wa manane pamoja na watu 4 waliokuwa naye.
Hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na serikali ya mapinduzi ya kijeshi kuhusu kukamatwa kwa Waziri wa zamani Swe.
Mbunge Win Htein, ambaye ni mwanachama mwandamizi wa NLD, pia alikamatwa mnamo Februari 5.
Jeshi la Myanmar lilipindua serikali ya utawala mnamo Februari 1, baada ya vikundi vya kisiasa vilivyo karibu nao kutoa madai ya udanganyifu katika uchaguzi wa tarehe 8 Novemba 2020 na mvutano kuongezeka nchini humo.
Wakati jeshi lilitangaza hali ya hatari kwa mwaka mmoja, maafisa wengi na viongozi wa chama tawala ikiwa ni pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na kiongozi halali wa nchi hiyo, Aung San Suu Kyi, walikamatwa.
Jumuiya ya kimataifa, haswa Umoja wa Mataifa (UN) na Jumuiya ya Ulaya (EU), walilaani mapinduzi hayo.
Uturuki pia imekuwa moja wapo ya nchi inayopinga vikali hali hiyo.
Marekani imeweka ajenda ya kurudisha vikwazo nchini Myanmar.
Wakati watu wakianza maandamano na kudai kurudishwa kwa demokrasia tangu Februari 6, polisi waliingilia kati na kukabiliana nao katika maeneo mengi.
Jeshi pia liliamua kuweka utawala wa kimabavu katika baadhi ya miji.

No comments:
Post a Comment