Shirika la Haki za Kibinadamu (HRW) limetangaza kuwa jeshi la Ethiopia lilitekeleza mauaji ya raia 83 katika mkoa wa Tigray, ambapo lilianzisha operesheni dhidi ya waasi.
Laetitia Bader ambaye ni Mkurugenzi wa HRW barani Afrika, alisema kuwa jeshi la Ethiopia liliharibu shule nyingi, nyumba na hospitali wakati wa operesheni iliyozinduliwa mnamo Novemba 2020, na kwamba raia 83 wakiwemo watoto miongoni mwao walipoteza maisha.
Akibainisha kuwa jeshi la Ethiopia lilishambulia makazi ya raia kiholela, Bader aliongezea kusema,
"Mashambulizi hayo yalisambaratisha maisha ya raia huko Tigray na kusababisha uhamiaji."
Kwa mujibu wa HRW, zaidi ya watu 200,000 huko Tigray walilazimika kuhama makazi yao kutokana na mzozo na kukimbilia katika nchi jirani ya Sudan.
Bader pia aliitaka serikali ya Ethiopia iwaruhusu waangalizi wa Umoja wa Mataifa (UN) kufanya uchunguzi wao huko Tigray.

No comments:
Post a Comment