Mkurugenzi wa Bodi ya Bonde la Maji ya Mto Pangani, Segule Segule amesema katika ukaguzi wao wamebaini kuwapo kwa maeneo ya vyanzo vya maji ambayo yamevamiwa.
"Katika ukaguzi wetu tumebaini baadhi ya maeneo ya vyanzo vya maji vinavyosimamiwa na bodi ya bonde la maji ya mto pangani ambayo yapo ndani vyanzo vya maji yamevamiwa na wananchi na tayari shughuli mbalimbali likiwemo kilimo, ufugaji na uvuvi haramu umekuwa ukifanywa," amesema Segule.
Amesema kuwa baadhi wananchi walioko ndani mita 60 kutoka vyanzo maji tayari wameshaelimishwa na kwamba hatua mbalimbali zimekwisha chukuliwa.
"Baadhi waliingia ndani ya vyanzo hivyo kwa kutokujua na wengi wanafahamu kabisa lakini tayari tumeshawaelimisha na kuwashauri, lengo ni kuhakikisha vyanzo hivyo vinakuwa endelevu," amesema Segule.
Kwa mujibu wa Segule, vyanzo vya maji zaidi 14 katika Mikoa ya Kanda ya Kaskazini vimekaguliwa na kuwekewa alama maalumu (bikon) lengo likiwa nikudhibithi uvamizi kwenye vyanzo na uharibifu wa mazingira.
No comments:
Post a Comment