Search This Blog

Sunday, February 21, 2021

Iran yasema inatafakari juu ya mkutano kati yake na Marekani

 


Naibu Waziri wa Mambo ya nje wa Iran Abbas Araqchi amesema nchi yake haijafikia uamuzi lakini inayatafakari mapendekezo ya Umoja wa Ulaya juu ya kufanyika mkutano usio rasmi kati ya wanachama wa sasa wa mkataba wa nyuklia wa mwaka 2015 ambapo Marekani iliyojitoa kwenye mkataba huo pia itashiriki. 


Iran na Marekani zimekuwa zikirushiana mpira kuhusu nani anapaswa kuchukua hatua ya kwanza ya kuyafufua mazungumzo juu ya mpango wa nyuklia wa Iran. 


Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump aliiondoa nchi yake kwenye mkataba huo na kuiwekea Iran vikwazo. Waziri wa Mambo ya nje wa Iran Mohammad Javad Zarif amesema mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Josep Borrell anaweza kuanzisha hatua za mazungumzo hayo. 


Wakati huo huo mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Uangalizi wa Nguvu za Nyuklia (IAEA), Rafael Grossi, aliwasili mjini Tehran siku ya Jumamosi, wiki chache baada ya bunge la Iran kutangaza tarehe ya mwisho ya Februari 23 kwa Marekani kuiondolea vikwazo nchi hiyo vinginevyo itasitisha shughuli za ukaguzi wa shirika la IAEA nchini humo.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...