Eneo la makutano ya barabara jijini Kinshasa limekuwa eneo lililovuta macho ya wengi baada ya kupatikana chuma cha ajabu, shirika la habari la Reuters limeripoti.
Watu wamekuwa wakichapisha picha ya chuma kinachong’aa ambapo vyuma kadhaa kama hivyo vimekuwa vikionekana duniani kote miezi ya hivi karibuni, cha kwanza huko Utah nchini Marekani mwezi Novemba mwaka jana.
‘’Tuliamka tukaona chuma hiki cha pembe nne,’’ Serge Ifulu, mkazi wa eneo hilo, aliliambia shirika la Reuters.
‘’Tulishangazwa kwasababu ni chuma ambacho huwa tunakiona kwenye Makala kuhusu freemasons au illuminati.’’

No comments:
Post a Comment