Search This Blog

Saturday, February 6, 2021

Biden amaliza mgogoro juu ya mwanamke wa kwanza mwafrika kuongoza WTO


Utawala wa Biden umemaliza mgogoro uliokuwa umetokea juu ya uteuzi wa mkuu wa Shirika la Biashara Duniani (WTO) kwa kumuunga mkono aliyekuwa waziri wa fedha nchini Nigeria.

Ngozi Okonjo-Iweala alikuwa anaongoza miongoni mwa waliokuwa wanawania wadhifa huo hadi mwezi Oktoba, utawala wa Trump uliposema kuwa haumuungi mkono badala yake unataka mwanamke mwingine wa Korea Kusini, Too Myung-hee kuchukua uongozi wa shirika hilo.

Bi. Yoo sasa amejiondoa kwenye kinyang'anyiro hicho.

Ikiwa itathibitishwa, Dkt. Okonjo-Iweala atakuwa mwanamke wa kwanza na mwafrika wa kwanza vilevile, kuongoza shirika la WTO.

Dkt. Okonjo-Iweala Ijumaa alimsifu mpinzani wake kwa ujumbe wake aliotoa na kusema: "Kuna kazi muhimu mbele yetu inayohitaji ushirikiano wetu pamoja."



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...