Utawala wa Biden umemaliza mgogoro uliokuwa umetokea juu ya uteuzi wa mkuu wa Shirika la Biashara Duniani (WTO) kwa kumuunga mkono aliyekuwa waziri wa fedha nchini Nigeria.
Ngozi Okonjo-Iweala alikuwa anaongoza miongoni mwa waliokuwa wanawania wadhifa huo hadi mwezi Oktoba, utawala wa Trump uliposema kuwa haumuungi mkono badala yake unataka mwanamke mwingine wa Korea Kusini, Too Myung-hee kuchukua uongozi wa shirika hilo.
Bi. Yoo sasa amejiondoa kwenye kinyang'anyiro hicho.
Ikiwa itathibitishwa, Dkt. Okonjo-Iweala atakuwa mwanamke wa kwanza na mwafrika wa kwanza vilevile, kuongoza shirika la WTO.
Dkt. Okonjo-Iweala Ijumaa alimsifu mpinzani wake kwa ujumbe wake aliotoa na kusema: "Kuna kazi muhimu mbele yetu inayohitaji ushirikiano wetu pamoja."

No comments:
Post a Comment