Search This Blog

Sunday, January 17, 2021

Wafanyakazi 4 wa meli ya mizigo ya Urusi wafariki baada ya kuzama Bartin


Wafanyikazi 4 wa meli ya mizigo yenye bendera ya Urusi iliyozama Bartin Inkumu walipoteza maisha na wengine 6 waliokolewa.

Taarifa zilizotolewa ziliripoti kuwa meli hiyo ilizama takriban mita 200 kutoka pwani ambapo  wafanyikazi 4 walipoteza maisha na watu wengine 6 waliokolewa na timu za Walinzi wa Pwani.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Gavana wa Bartın, juhudi za utafutaji na uokoaji wa wafanyikazi wengine waliokuwa kwenye meli zinaendelea.

Wizara ya Ulinzi ya Kitaifa pia ilitangaza kwamba vikosi vya frigate vilipewa agizo na Kamandi wa Vikosi vya Wanamaji kusaidia juhudi za utaftaji na uokoaji.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...