Search This Blog

Thursday, January 28, 2021

Mawaziri wa mambo ya kigeni na ulinzi wa Ujerumani na Marekani wafanya mazungumzo


Mawaziri wa ulinzi na mambo ya kigeni wa Marekani na Ujerumani wamefanya mazungumzo kwa njia ya simu na kuahidi mwanzo mpya baada ya enzi ya Donald Trump iliyolemaza mahusiano kati ya Washington na Berlin. 

Kwenye mazungumzo na mwenzake wa Ujerumani Annegret Kramp-Karrenbauer, waziri mpya wa ulinzi wa Marekani Lloyd Austin ameisifu Ujerumani kwa kuwa mwenyeji wa vikosi vya nchi yake na kuashiria kuwa atapitia upya uamuzi wa utawala uliopita wa kuondoa karibu theluthi ya wanajeshi wa Marekani nchini Ujerumani. 

Uamuzi huo wa utawala wa Trump uliishangaza Ujerumani ambayo haikujumishwa kwenye majadiliano na ulitishia kuteteresha zaidi mahusiano baina ya mataifa hayo mawili wanachama wa Jumuiya ya NATO.

 Kwa upande wake waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Heiko Maas aliyezungumza na mwenzake wa Marekani Antony Blinken wamekubaliana kufanya kazi pamoja katika masuala ya kuikabili China na uwezo wa nyuklia wa Iran.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...