Search This Blog

Saturday, December 19, 2020

Watu 21 wauawa kwenye shambulio la kujitoa muhanga nchini Somalia

 


Idadi ya watu waliouawa kwenye shambulio la bomu katika mji wa Galkayo nchini Somalia imeongezeka na kufikia watu 21. 

Kundi la kigaidi la Al Shabaab limedai kuhusika na mashambulio hayo. Msemaji wa serikali ya jimbo la Gamudung amesema wengi waliouawa ni wanajeshi wakiwemo makamanda watatu wa kijeshi baada ya mshambuliaji wa kujitoa muhanga kujilipua. 

Watu wengine 19 walijeruhiwa kwenye shambulio hilo. Waziri Mkuu wa Somalia Hussein Roble alihudhuria mazishi ya wanajeshi waliouawa kwenye mlipuko huo na amelaani tukio hilo ambalo aliliita la kigaidi. 

Mlipuko huoulitokea karibu na uwanja wa michezo siku ya Ijumaa ambapo watu walikuwa wamekusanyika kwa ajili ya kumkaribisha waziri mkuu Roble. Kundi la Al shabaab limesema mlengwa hasa alikuwa ni waziri Mkuu huyo wa Somalia.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...