Search This Blog

Saturday, December 26, 2020

Nigeria: Boko Haram wawaua wanavijiji mkesha wa Krismasi


Watu kadhaa wameuawa kaskazini mashariki mwa Nigeria baada ya wanamgambo wa Boko Haram kushambulia vijiji vya Wakristo na kuteketeza Kanisa mkesha wa Krismasi.

Wapiganaji waliingia Pemi katika jimbo la Borno, kwa kutumia magari na piki piki na kuanza kufyatua risasi kiholela, mmoja wa viongozi katika kijiji hicho aliambia shirika hilo la habari.

Pemi iko karibu na Chibok ambako wasichana 200 wa shule walitekwa mwaka 2014.

Boko Haram wamefanya mashambulio kadhaa kaskazini mwa Nigeria ambako wanapigana kupindua serikali ili kubuni taifa la Kiislamu.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...