Search This Blog

Monday, December 7, 2020

Idadi ya vifo vya raia yaongezeka Yemen


Idadi ya raia wanaopoteza maisha kutokana na vita vya ndani nchini Yemen inaendelea kuongezeka kila siku.

Ofisi ya Uratibu wa Masuala ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (UN) ilitangaza kuwa raia 139 waliuawa na kujeruhiwa katika miezi miwili iliyopita katika eneo la Hudayda kutokana mizozo iliyoongezeka.

Katika taarifa iliyotolewa na ofisi hiyo, ilisisitizwa kuwa pande zote zinazozozana zinapaswa kuacha mashambulizi dhidi ya raia ambayo yanakiuka sheria za kimataifa.

Hafi kufikia sasa tangu kuanza kwa vita vya ndani vya Yemen, raia 12,000, na jumla ya watu 112,000 wamepoteza maisha.

Miongoni mwa watu waliopoteza maisha kuna watoto 2,138.

Wakati huo huo, kamanda mwandamizi kutoka Baraza la Mpito la Kusini aliyekuwa akiungwa mkono na serikali ya Abu Dhabi, aliuawa katika mji wa Ebyen.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...