Mahakama Kuu, Dar es Salaam, imetengua hukumu iliyoamuru kampuni ya simu za mkononi MIC (T) Limited, maarufu Tigo, kuwalipa wanamuziki wa kizazi kipya Hamisi Mwinyijuma (Mwana-FA) na Ambwene Yesaya (AY) Sh2.1 bilioni kwa kukiuka sheria za hatimiliki.
Jaji Joacquine De-Mello amebatilisha uamuzi huo baada ya kukubaliana na rufaa ya Tigo kuwa Mahakama ya Wilaya ya Ilala haikuwa na mamlaka ya kisheria kusikiliza kesi hiyo.

No comments:
Post a Comment