Search This Blog

Thursday, December 17, 2020

Gavana Sonko wa Nairobi aondolewa madarakani


Bunge la Seneti nchini Kenya limepiga kura kumuondoa Mike Mubuvi Sonko kama gavana wa Nairobi , katika hatua ambayo imekomesha miaka mitatu ya utawala wake uligubikwa na utata.

Bw. Sonko anatuhumiwa kwa ukiukaji wa katiba, utumizi mbaya wa mamlakaa, utovu wa nidhamu, na uhalifu chini ya sheria.

Maseneta 27 walipiga kura kuunga mkono kuondolewa ofisini kwa Bw Sonko kwa kudumisha mashtaka yote manne yaliyowasilishwa na Bunge la Kaunti ya Nairobi, ambalo lilipiga kura ya kutokuwa na imani naye mnamo Desemba 3.

Kuondolewa madarakani kwa Bw. Sonko kumetoa nafasi kwa Spika wa Bunge la Kaunti ya Nairobi Ben Mutura kushikilia wadhifa huo hadi uchaguzi wa gavana na naibu wake utakapofanywa katika kipindi cha siku 60 zijazo.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...