Search This Blog

Tuesday, November 17, 2020

Urusi inapanga kujenga kambi ya jeshi lake Sudan


Rais wa Urusi Vladimir Putin ameidhinisha kuendelezwa kwa makubaliano na Sudan ya kuanzishwa kwa kambi ya jeshi katika pwani ya Bahari Nyekundi.

Urusi inapanga kujenga kituo cha usafirishaji na ukarabati kwa jeshi lake la majini ambacho kitakuwa na wafanyakazi wasiozidi 300.

Rasimu ya makubaliano ya kambi hiyo itakuwa viungani mwa kaskazini mwa Bandari ya Sudan.

Wachambuzi wanasema, Urusi imeongeza shughuli zake Afrika katika miaka ya hivi karibuni hatua inayochukuliwa kama njia moja ya kupunguza ushawishi wa China na Marekani barani humo.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...