Search This Blog

Tuesday, November 17, 2020

Barabara ya Jangwani yafungwa kutokana na mafuriko


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wakala wa Mabasi yaendayo haraka Dar es Salaam (DART), imeeleza kuwa, njia ya Jangwani imefungwa kutokana na mafuriko ya maji hii leo Novemba 17, 2020, kuanzia saa 3:30 asubuhi, na huduma ya mabasi hayo inaendelea kupitia njia ya Kigogo na Mkwajuni.

Taarifa hiyo imetolewa leo Novemba 17, 2020, kupitia ukurasa wa Twitter wa Wakala wa mabasi hayo.

"Njia ya Jangwani imefungwa kutokana na mafuriko ya maji leo, Jumanne, Novemba 17, 2020, kuanzia saa 3:30 asubuhi, huduma ya mabasi ya DART inaendelea kupitia njia ya Kigogo na Mkwajuni ili kufika Kariakoo, Kimara, Morocco, Kivukoni na sehemu nyingine za jiji la Dar es Salaam", imeeleza taarifa hiyo.

 




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...